ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 11 Mei 2015

New S. African Democratic Alliance Leader Rejects ‘Token Black' Label

Newly-elected Democratic Alliance (DA) party leader Mmusi Maimane, delivers his victory speech May 10, 2015, in Port Elizabeth, South Africa.
Newly-elected Democratic Alliance (DA) party leader Mmusi Maimane, delivers his victory speech May 10, 2015, in Port Elizabeth, South Africa.
South Africa's main opposition party, the Democratic Alliance (DA), has elected its first black leader.  Mmusi Maimane takes over from Helen Zille, who has been at the helm of the party for eight years.
At 34 years of age, the charismatic politician known for his sharp oratory skills and slick campaigns is often dubbed the “Obama of Soweto."
Mmusi Maimane pushes away such comparisons, but observers say his appointment as the new leader DA party could help shift a political landscape that currently tilts heavily in favor of the ruling African National Congress (ANC) party.
The eldest of four siblings, Maimane was born in Krugersdorp and brought up in Soweto - a township on the edges of Johannesburg that became the political epicenter of the anti-apartheid struggle.
Maimane joined the DA in 2010. He quickly rose through the ranks to become the party’s national spokesman in 2011.  Last year, he lost his bid to lead the provincial government of South Africa's wealthiest province, Gauteng.
As the party's parliamentary leader, he accused President Jacob Zuma of being a “thief” during a heated parliamentary debate in March.  His colleagues say he has a good sense of humor but is an “absolute perfectionist."
On May 10, Maimane became the DA’s first black party leader during a party conference with 88.9 percent of the vote.
Despite the DA’s growth in the last few elections – 12.4 percent of the vote in 2004, 16.7 percent in 2009 and 22.2 percent in 2014 – the party is still considered “too white” to threaten the supremacy of the ruling ANC, says political analyst Nic Borain.
Electing Maimane as party leader is one of several steps the DA is taking to enable it to dig into the ANC’s core constituency, Borain says.
“Mmusi is very specifically tailored.  He was chosen and his rise was so quick because he fits exactly the profile the DA wants.  His appointment is a necessary but not sufficient condition for the DA to break out of its racial confines.  Mmusi is the transitional object,” says Borain.
Maimane has a bachelor's degree in psychology from the University of South Africa and a master’s degree in theology from Bangor University in the United Kingdom.
Before getting into politics, the gangly, eloquent leader - included in GQ magazine's 2014 list of best-dressed men - lectured at a business school in Johannesburg.  A devout Christian, he is a preacher at the charismatic Discovery Church in Randburg.
Borain says it’s Maimane’s “popular appeal” the DA is hoping to capitalize on.
“Electing a leader who is a preacher in charismatic churches is a particular kind of appeal which the DA historically shied away from – a popular appeal.  I think it is part of the compromises the DA is prepared to make with its principled ideology historically to reach new voters, new young black voters,” says Borain.
The ANC has said that he is too young and that his rapid elevation is a symptom of racial tokenism – a label flatly rejected by Maimane’s colleague and shadow minister for public enterprises, Natasha Michaels.
“Calling Mmusi a token black is an absolute insult.  I think the fact that he received the overwhelming landslide victory that he did proves that black, white, colored, Indian, Asian – we all agreed that he was the man for the job and he was the man to take us forward,” said Michaels. “The energy of his age is going to be a huge advantage. He brings a certain dynamic to parliament that is desperately needed because we are a very young country," added Michaels.(source VOICE OF AMERICA)

Ijumaa, 8 Mei 2015

SHERIA YA MAKOSA YA MITANDAO TAYARI IMESAINIWA NA RAIS

Rais Jakaya Kikwete tayari ameshasaini sheria yenye utata ya makosa ya mtandao na muda wowote kuanzia sasa itaanza kutumika rasmi
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, amesema hayo leo wakati akizungumzia masuala mbali mbali yanayohusu sheria hiyo ambayo kupitishwa kwake kumesababisha malalamiko mengi kutoka kwa wadau kuwa itaminya uhuru wa habari, kuingilia faragha pamoja na uhuru wa watu kuwasiliana.
Huu ni uchambuzi kidogo kuhusu baadhi ya vipengele vilivyozua utata katika muswada uliokuwa umetolewa
1. Kifungu 7 (2b): Mpokeaji wa ujumbe (receiver) anaweza kushtakiwa kwa kosa la kupokea ujumbe ambao sheria imeufanya kuwa wa jinai. (Mfano: Mtu akikuforwadia ujumbe, ukiupokea na wewe umefanya kosa la jinai).
2. Kifungu 8: Itakuwa ni kosa la jinai kama mtu ataweka wazi nyaraka za siri za serikali hata kama ni nyaraka ya kusaidia nchi kwa ujumla (Mfano: Matumizi mabaya ya mali ya umma).
3. Kifungu 14: Picha yoyote yenye mwelekeo unaoweza kuonekana kama ‘mchafu kingono’ inaweza kupelekea mtu kufungwa hadi miaka 10 au kulipa milioni 30; (Mfano: mtu kaposti picha yake ambayo sio ya ponografia lakini ‘ikatafsiriwa’ hivyo. Sheria haijatafsiri ponografia!)
4. Kifungu 23: Je, ulijua kuwa ‘kusababisha maudhi ya hisia’ kwa mtu mwingine ni unyanyasaji na unaweza kufungwa kifungo kisichopungua mwaka mmoja?
5 Kifungu 22: Ukiweka ujumbe katika mtandao na ukaufuta au kuuboresha, kama ukishtakiwa kwa kuweka ujumbe huo unaweza kuhukumiwa pia kwa adhabu ya kuuboresha au kuufuta. (Mfano: unapofuta ‘status’ zako za WhatsApp, unaweza shitakiwa kwa kuchelewesha ushahidi kisa tu ulifuta na hamna mtu anayeweza kujua ulifuta kwa kusudi au la.)
6. Mkuu wa kituo cha Polisi chochote kile nchini anaweza kuagiza wewe umpatie simu/laptop yako au taarifa zako zote (kwenye email, chats) au hata vifaa vyako au ofisi yako kwa ajili ya upelelezi bila oda ya Mahakama.
7. Serikali kupitia waziri husika ndio ina mamlaka ya kusema jambo lililowekwa kwenye mtandao ni la kweli, uongo au la kupotosha(SOURCE:East Africa Television (EATV)

Alhamisi, 7 Mei 2015

huyo ndo rais mpya aliyechaguliwa DARUSO-MUCE

SHAMRA SHAMRA ZA USHINDI 
 Baada ya kampeni zilizo dumu kwa wiki moja, wanafunzi wa chuo kikuu Dar es salaam kitivo cha uwalimu Iringa (MUCE) wamefanya uchaguzi leo, Kwa hali ya amani na utulivu wa hali ya juu na hatimaye kuwapata viongozi wa serikali yao, Uchaguzi huo uliokuwa unawagombea zaidi wawili  katika kila nafasi ulilazimu kuwachukuwa siku nzima kufanyika na hatimaye Bw. BAKARI, IBRAHIMU ameibuka mshindi katika nafasi ya urais, Kwa matokeo mengine ungana nasi kesho

 

Mrema avuliwa uanachama TLP

Mrema avuliwa uanachama TLP

mrema
NA SHABANI MATUTU, DAR ES SALAAM
KAMATI ya Ukweli na Maridhiano ya Chama cha Tanzania Labour (TLP), imetangaza kumvua uanachama Mwenyekiti wa chama hicho, Agustino Mrema.
Akizungumza jana, jijini Dar es Salaam na MTANZANIA Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Joram Kinanda alisema kuwa kamati hiyo imefikia uamuzi huo baada ya kupitia kwa kina malalamiko yaliyokuwa yakimuhusu Mrema, ambaye pia ni Mbunge wa Vunjo.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa mbali na Mrema wengine waliovuliwa uanachama ni Hamisi Mkadamu, Antoni Mapunda, Nancy Mrikaria, Dominata Rwechungura, Maxmilian Lymo, Richad Lyimo, Hamisi Mkumba na Stanley Temba.
Kinanda alisema kuwa wanachama hao wamevuliwa uanachama kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, toleo la 2005 Ibara ya 9.9 (c) na 2009 ibara 9.5(c).
Kinanda alisema kuwa maazimio hayo yamepelekwa katika ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kwa taratibu za kisheria pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Kwa upande wake Msajili Msaidizi wa Vyama Vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza, alipotafutwa ili kupata ufafanuzi wa suala hilo, alisema kamati hiyo haitambuliki kisheria.
“Kamati hiyo haitambuliki kisheria, na hata Mrema mwenyewe amekuwa akipinga TLP kuwa na kamati ya aina hiyo na hata viongozi wake hawatambuliki, ” alisema(Chanzo Mtanzania)


Jumanne, 5 Mei 2015

Madereva wasitisha mgomo, mabasi ya mikoani yaanza kazi


Mbowe akizungumza na madereva mara baada ya kuwasili katika kituo cha mabasi cha Ubongo leo jijini Dar es Salaam.  
Na Online Team, Mwananchi

Posted  Jumanne,Mei5  2015  saa 8:24 AM
Kwa ufupi
Mgomo huo ulioanza jana umesababisha usumbufu mkubwa kwa raia sehemu nyingi nchini Tanzania ambao walikuwa wamejiandaa kusafiri kuelekea katika mikoa mingine jana na leo kwa ajili ya shughuli zao mbalimbali zikiwemo za kibiashara na kijamii.
Hatimaye madereva wa mabasi na malori wameamua kusitisha mgomo leo baada ya Serikali kuwahakikishia kuwa inaandaa utaratibu mzuri wa kujibu na kushughulikia matatizo yao.
Mgomo huo ulioanza jana umesababisha usumbufu mkubwa kwa raia sehemu nyingi nchini Tanzania ambao walikuwa wamejiandaa kusafiri kuelekea katika mikoa mingine jana na leo kwa ajili ya shughuli zao mbalimbali zikiwemo za kibiashara na kijamii.
Taarifa zilizotufikia ni kwamba Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akiwa na viongozi wengine wa Serikali walifika katika kituo cha mabasi yaendao mikoani cha ubungo na kuzungumza na madereva hao wakiwataka wasitishe mgomo wao na kuanza kazi kwani mambo yao Serikali inayafanyia kazi na hivi karibuni watajibiwa.
Kufuatia hali hiyo maderva hao walikubaliana na ombi hilo la Serikali baada ya kutokea kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe ambaye naye aliwasihi waache mgomo huo kwani Serikali itafanyia kazi maombi yao.
Nchi yasimama: Madereva mabasi, malori wagoma sehemu kubwa ya Tanzania
Dar/mikoani. Nchi imesimama. Hii ndiyo sentensi inayofaa kuelezea tukio la jana la mgomo wa madereva nchini kote ambao kwa mara ya kwanza ulisababisha mabasi yote kutoka Dar es Salaam kwenda mikoani na nchi jirani kushindwa kuondoka.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT), kushindwa kutoa huduma kwa sababu yoyote ile.
Tangu asubuhi hadi jioni, hakuna basi hata moja lililotoka wala kuingia katika kituo hicho hadi abiria walipoanza kukata tamaa na baadhi yao kuondoka na wengine kuanza kushinikiza kurejeshewa nauli.
Mgomo huo ambao ni mwendelezo wa ule uliofanyika Aprili 9, mwaka huu ulipewa uzito na madereva hao baada ya ahadi walizopewa na Serikali kutofanyiwa kazi kama ilivyoahidiwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka.

Hata hivyo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameunda kamati ya iliyotangazwa na Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta ya kusimamia usafiri barabarani itakayowakutanisha wadau wote ili kutatua matatizo katika sekta hiyo kila yanapotokea.
Polisi wachemsha Dar
Tangu saa 2.30 asubuhi, polisi walijaribu kuyasindikiza mabasi waliyodhani madereva wake wako tayari kuondoka Ubungo lakini walishindwa baada ya kutoungwa mkono.
Mkuu wa Trafiki Ubungo, Inspekta Yussuf Kamotta akiwa na Inspekta Solomon Nkindwa ambaye pia ni mkaguzi wa magari, waliingia katika basi la Kampuni ya Master City na kuliondoa kituoni hapo wakiwa na mmiliki wa kampuni hiyo, Abdallah Mohammed huku wakimtafuta dereva bila mafanikio na kulazimika kulitafutia sehemu salama ya kuliegesha baada ya madereva kulizingira.
Kitendo cha askari hao kilisababisha kuzomewa kwa Inspekta Nkindwa wakisema mkaguzi huyo arudi shule akasome... “Solomoooon… rudi shuuuule… gia nane… zimekushinda,” walisikika madereva hao wakiimba huku wakikimbia mchakamchaka kurudi zilipo ofisi zao.
Kutokana na vurugu zilizotokea nje ya kituo hicho, polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya watu waliokuwa katika makundi.
Nje ya UBT, magari sita ya polisi yaliegeshwa katika makutano ya barabara za Sam Nujoma, Nelson Mandela na Morogoro wakati mengine yakielekea Mwenge na Buguruni kwenda kukabiliana na tishio lolote ambalo lingeweza kutokea.
Saa 5.30 askari wa Kikosi cha Mbwa waliwasili kuongeza nguvu na kuvutia macho ya wengi kutokana na jinsi walivyokuwa na pilikapilika bila ya kuwapo kwa mhalifu yeyote anayetafutwa.
Sikukuu ya madereva
Tofauti na migomo mingine, huu haukuwa na vurugu zozote wala sintofahamu kwani kila mtu aliyekuwa UBT alionekana akiwa katika sehemu yake akiendelea na hamsini zake. Abiria walikuwa katika mabasi husika huku mawakala na makarani wakiendelea kukatisha tiketi za safari na kupanga mizigo ya abiria.
Huku wakiendelea na mazungumzo yao katika vikundi katika kituo hicho, madereva hao walisikia wakisema hapakuwa na mgomo, bali sikukuu yao.(CHANZO MWANANCHI)

ANGALIZO ..............

Ndugu watazamaji wa blog hii, blog hii imeanzishwa kwa lengo la kufikisha ujumbe kwa jamii,kutoa taarifa na kuonya,  kutoa maoni na kama unatangazo lolote huna budi kuwasiliana nasi 

lakini sio kutaka kile wanachokitaka watu wachache kwa hiyo kama kuna tatizo wasiliana nasi na si kulaumu na kuchafua chombo husika, .

TANGAZA BIASHARA, TAARIFA NA MAELEZO WASILIANA NASI.

Jumamosi, 2 Mei 2015

KAMPENI ZA UCHAGUZI KUTOKA CHUO KIKUU KISHIRIKI MKWAWA 2015

KAMPENI ZA UCHAGUZI KUWANIA UONGOZI KATIKA SERIKALI YA WANAFUNZI ZAENDELEA KWA MBWEMBWE

 

Serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Mkwawa (DARUSO-MUCE) imemaliza muda wake na hivyo iko katika mchakato wa kutafuta Rais mpya wa serikali hiyo pamoja na wabunge watakaongoza serikali hiyo kwa kipindi cha 2015/16 Chuoni hapo.
Aidha kampeni za mgombea Urais ndugu BAKARI, IBRAHIMU zimeonekana  kuwawavutia wanafunzi wengi kwani amekuwa akitembelea wapiga kura wake huku akiwa ameandamana na wafuasi  wake ambao wamekuwa wakimlinda kila anapokwenda. Aidha mgombea huyo Bw. BAKARI, IBRAHIMU ndie ambae anaonekana ni mwenye asilimia kubwa ya kuweza kushinda katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika wiki lijalo chuoni hapo. Wagembea wengine ni; MSUYA, FAROUK na Bw MABULA

WAGOMBEA URAIS DARUSO MUCE 2015/2016.....................

Na kwa upande wa makamu wa rais wagombea wawili wamejitokeza  akiwamo dada ISSASSI SUZANI na KIBONA FAUSTA katika nafasi hii ushindani unaonekana kuwa ni mkubwa sana kwani wote wana watu weng wanaowapigania ili kupata nafasi hiyo




WAGOMBEA WA NAFASI YA MAKAMU WA RAIS DARUSO-MUCE 2015/2016

Mgombea wa nafasi ya Rais Bwana BAKARI, IBRAHIMU  sera zake kwa wapiga kura (hawapo pichani) ambapo alisema katika uongozi wake ataanza kushughulikia mikopo kwa wanafunzi wa MUCE.
Pia amesema kama atapewa nafasi hiyo atakuwa na utaratibu wa kuwakutanisha wanafunzi wa MUCE kuanzia mwaka wa kwanza mpaka wa tatu na wataalumu waliopo katika fani zao, lengo likiwa ni kuwaongezea uzoefu zaidi na kujua changamoto ya kazi za kitaaluma chuoni hapo.
Aidha aliongeza kuwa atahakikisha usiri wa matokeo utaboreshwa chuoni hapo, huku akimwaga ahadi ya hakuna tatizo ambalo hawezi kulishughurikia akiwa rais na hii ilikuja baada ya mheshimiwa kitako kumuuliza mgombea matatizo gani manne(4)  hawezi kuwasaidia wanachuo akiwa madarakani.

Wanafunzi hao wameonekana wana ukomavu mkubwa wa kisiasa kwani wanasikiliza kwa makini sera za wagombea na kuuliza  maswali mazuri.
Cha kufurahisha ni kelele za filimbi na mayowe ambayo yametwala kila kona huku wagombea wakishangiliwa na mashabiki wao.

Nafasi zinazowaniwa katika Uchaguzi huo ni pamoja na nafasi ya Rais, Makamu wa Rais, pamoja na wawakilishi wa Vitivo (wabunge) na wawakilishi wa Maeneo (wabunge wa makazi) ambao wote watapigiwa kura.
Wagombea mbalimbali wamekuwa wakipita hapa na pale ikiwa ni pamoja na kubandika picha zao katika kuta ikiwa ni sehemu ya kutafuta kura.
Kwa upande wa MSUYA  naye amenadi sera sake moja ya mipango yake ni kushughulikia matatizo mbalimbali ya wanafunzi likiwemo tatizo la maji na tatizo la umeme kukatika mara kwa mara, huku akiwasii wanafunzi kuangalia hali ya chou sasa kwamba kinahitaji mtu makini anayejua matatizo ya wanachuo wote na kuwatumikia.
KWA UPANDE WA MAKAMU WA RAIS SERA ZAO IMEONEKANA KWENDA SAMBAMBA NA MARAIS lengo kubwa ni kuboresha taaluma na mazingira y chuoni hapo.

Kwa upande wake Rais anayemaliza muda wake Bwana AGUSTINO ALFA ameishukuru tume ya uchaguzi kwa mchakato mzima na anafurahi kumaliza muda wake na kuwataka watakaopata nafasi za kuongoza wazingatie sheria, demokrasia na upendo ili kuleta mshikamano katika chuo, ili wanaoongozwa wajisikie kuwa na amani kuwepo chuoni hapo badala ya kutatua migogoro isiyokuwa na maana. Pia ameshauri wanachuo kusikiliza sera za wagombea kwa umakini mkubwa ili kuepuka KUUZIWA MBUZI KWENYE GUNIA.
 
 MSHAURI WA WANAFUNZI ALITUMIA FURSA HIYO KUWAASA WAGOMBEA KUTUNZA MAZINGIRA HASA KUTOBANDIKA MABANGO SEHEMU ZISIZO RASMI
                                         NAYE MAKAMU WA CHUO AKASEMA;
Makamu mkuu wa chuo amewatakia wanafunzi kampeni njema zenye baraka na fanaka na zinazozingatia sheria na taratibu za chuo.