KAMPENI ZA UCHAGUZI KUWANIA UONGOZI KATIKA SERIKALI YA WANAFUNZI ZAENDELEA KWA MBWEMBWE
Serikali ya wanafunzi ya Chuo 
Kikuu cha Mkwawa (DARUSO-MUCE) imemaliza muda wake na hivyo iko katika mchakato
 wa kutafuta Rais mpya wa serikali hiyo pamoja na wabunge watakaongoza 
serikali hiyo kwa kipindi cha 2015/16 Chuoni hapo. 
Aidha kampeni za mgombea Urais
 ndugu BAKARI, IBRAHIMU zimeonekana  kuwawavutia wanafunzi wengi kwani 
amekuwa akitembelea wapiga kura wake huku akiwa ameandamana na wafuasi  
wake ambao wamekuwa wakimlinda kila anapokwenda. Aidha mgombea huyo Bw. BAKARI, IBRAHIMU  ndie ambae anaonekana ni mwenye asilimia kubwa ya kuweza 
kushinda katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika wiki lijalo chuoni hapo. Wagembea wengine ni; MSUYA, FAROUK na Bw MABULA
WAGOMBEA URAIS DARUSO MUCE 2015/2016.....................
Na kwa upande wa makamu wa rais wagombea wawili wamejitokeza  akiwamo dada ISSASSI SUZANI na KIBONA FAUSTA katika nafasi hii ushindani unaonekana kuwa ni mkubwa sana kwani wote wana watu weng wanaowapigania ili kupata nafasi hiyo
WAGOMBEA WA NAFASI YA MAKAMU WA RAIS DARUSO-MUCE 2015/2016
Mgombea wa nafasi ya Rais Bwana BAKARI, IBRAHIMU  sera 
zake kwa wapiga kura (hawapo pichani) ambapo alisema katika uongozi wake
 ataanza kushughulikia mikopo kwa wanafunzi wa MUCE.
Pia amesema kama atapewa nafasi hiyo 
atakuwa na utaratibu wa kuwakutanisha wanafunzi wa MUCE kuanzia mwaka wa
 kwanza mpaka wa tatu na wataalumu waliopo katika fani zao, lengo likiwa
 ni kuwaongezea uzoefu zaidi na kujua changamoto ya kazi za kitaaluma chuoni hapo.
Aidha aliongeza kuwa atahakikisha usiri wa matokeo utaboreshwa chuoni hapo, huku akimwaga ahadi ya hakuna tatizo ambalo hawezi kulishughurikia akiwa rais na hii ilikuja baada ya mheshimiwa kitako kumuuliza mgombea matatizo gani manne(4)  hawezi kuwasaidia wanachuo akiwa madarakani.
Wanafunzi hao wameonekana wana ukomavu mkubwa wa kisiasa kwani wanasikiliza kwa makini sera za wagombea na kuuliza  maswali mazuri.
Cha kufurahisha ni kelele za filimbi na mayowe ambayo yametwala kila kona huku wagombea wakishangiliwa na mashabiki wao.
Nafasi
 zinazowaniwa katika Uchaguzi huo ni pamoja na nafasi ya Rais, Makamu wa
 Rais, pamoja na wawakilishi wa Vitivo (wabunge) na wawakilishi wa 
Maeneo (wabunge wa makazi) ambao wote watapigiwa kura.
Wagombea
 mbalimbali wamekuwa wakipita hapa na pale ikiwa ni pamoja na kubandika 
picha zao katika kuta ikiwa ni sehemu ya kutafuta kura.
Kwa upande wa MSUYA  naye amenadi sera sake moja ya mipango yake ni kushughulikia matatizo mbalimbali ya wanafunzi likiwemo tatizo la maji na tatizo la umeme kukatika mara kwa mara, huku akiwasii wanafunzi kuangalia hali ya chou sasa kwamba kinahitaji mtu makini anayejua matatizo ya wanachuo wote na kuwatumikia.
KWA UPANDE WA MAKAMU WA RAIS SERA ZAO IMEONEKANA KWENDA SAMBAMBA NA MARAIS lengo kubwa ni kuboresha taaluma na mazingira y chuoni hapo.
Kwa upande wake Rais 
anayemaliza muda wake Bwana AGUSTINO ALFA ameishukuru tume ya uchaguzi 
kwa mchakato mzima na anafurahi kumaliza muda wake 
na kuwataka watakaopata nafasi za kuongoza wazingatie sheria, demokrasia
 na upendo ili kuleta mshikamano katika chuo, ili wanaoongozwa wajisikie
 kuwa na amani kuwepo chuoni hapo badala ya kutatua migogoro isiyokuwa 
na maana. Pia ameshauri wanachuo kusikiliza sera za wagombea kwa umakini mkubwa ili kuepuka KUUZIWA MBUZI KWENYE GUNIA.
 MSHAURI WA WANAFUNZI ALITUMIA FURSA HIYO KUWAASA WAGOMBEA KUTUNZA MAZINGIRA HASA KUTOBANDIKA MABANGO SEHEMU ZISIZO RASMI
                                         NAYE MAKAMU WA CHUO AKASEMA; 
Makamu mkuu wa chuo amewatakia wanafunzi kampeni njema zenye baraka na fanaka na zinazozingatia sheria na taratibu za chuo.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni