ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 2 Mei 2015

KAMPENI ZA UCHAGUZI KUTOKA CHUO KIKUU KISHIRIKI MKWAWA 2015

KAMPENI ZA UCHAGUZI KUWANIA UONGOZI KATIKA SERIKALI YA WANAFUNZI ZAENDELEA KWA MBWEMBWE

 

Serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Mkwawa (DARUSO-MUCE) imemaliza muda wake na hivyo iko katika mchakato wa kutafuta Rais mpya wa serikali hiyo pamoja na wabunge watakaongoza serikali hiyo kwa kipindi cha 2015/16 Chuoni hapo.
Aidha kampeni za mgombea Urais ndugu BAKARI, IBRAHIMU zimeonekana  kuwawavutia wanafunzi wengi kwani amekuwa akitembelea wapiga kura wake huku akiwa ameandamana na wafuasi  wake ambao wamekuwa wakimlinda kila anapokwenda. Aidha mgombea huyo Bw. BAKARI, IBRAHIMU ndie ambae anaonekana ni mwenye asilimia kubwa ya kuweza kushinda katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika wiki lijalo chuoni hapo. Wagembea wengine ni; MSUYA, FAROUK na Bw MABULA

WAGOMBEA URAIS DARUSO MUCE 2015/2016.....................

Na kwa upande wa makamu wa rais wagombea wawili wamejitokeza  akiwamo dada ISSASSI SUZANI na KIBONA FAUSTA katika nafasi hii ushindani unaonekana kuwa ni mkubwa sana kwani wote wana watu weng wanaowapigania ili kupata nafasi hiyo




WAGOMBEA WA NAFASI YA MAKAMU WA RAIS DARUSO-MUCE 2015/2016

Mgombea wa nafasi ya Rais Bwana BAKARI, IBRAHIMU  sera zake kwa wapiga kura (hawapo pichani) ambapo alisema katika uongozi wake ataanza kushughulikia mikopo kwa wanafunzi wa MUCE.
Pia amesema kama atapewa nafasi hiyo atakuwa na utaratibu wa kuwakutanisha wanafunzi wa MUCE kuanzia mwaka wa kwanza mpaka wa tatu na wataalumu waliopo katika fani zao, lengo likiwa ni kuwaongezea uzoefu zaidi na kujua changamoto ya kazi za kitaaluma chuoni hapo.
Aidha aliongeza kuwa atahakikisha usiri wa matokeo utaboreshwa chuoni hapo, huku akimwaga ahadi ya hakuna tatizo ambalo hawezi kulishughurikia akiwa rais na hii ilikuja baada ya mheshimiwa kitako kumuuliza mgombea matatizo gani manne(4)  hawezi kuwasaidia wanachuo akiwa madarakani.

Wanafunzi hao wameonekana wana ukomavu mkubwa wa kisiasa kwani wanasikiliza kwa makini sera za wagombea na kuuliza  maswali mazuri.
Cha kufurahisha ni kelele za filimbi na mayowe ambayo yametwala kila kona huku wagombea wakishangiliwa na mashabiki wao.

Nafasi zinazowaniwa katika Uchaguzi huo ni pamoja na nafasi ya Rais, Makamu wa Rais, pamoja na wawakilishi wa Vitivo (wabunge) na wawakilishi wa Maeneo (wabunge wa makazi) ambao wote watapigiwa kura.
Wagombea mbalimbali wamekuwa wakipita hapa na pale ikiwa ni pamoja na kubandika picha zao katika kuta ikiwa ni sehemu ya kutafuta kura.
Kwa upande wa MSUYA  naye amenadi sera sake moja ya mipango yake ni kushughulikia matatizo mbalimbali ya wanafunzi likiwemo tatizo la maji na tatizo la umeme kukatika mara kwa mara, huku akiwasii wanafunzi kuangalia hali ya chou sasa kwamba kinahitaji mtu makini anayejua matatizo ya wanachuo wote na kuwatumikia.
KWA UPANDE WA MAKAMU WA RAIS SERA ZAO IMEONEKANA KWENDA SAMBAMBA NA MARAIS lengo kubwa ni kuboresha taaluma na mazingira y chuoni hapo.

Kwa upande wake Rais anayemaliza muda wake Bwana AGUSTINO ALFA ameishukuru tume ya uchaguzi kwa mchakato mzima na anafurahi kumaliza muda wake na kuwataka watakaopata nafasi za kuongoza wazingatie sheria, demokrasia na upendo ili kuleta mshikamano katika chuo, ili wanaoongozwa wajisikie kuwa na amani kuwepo chuoni hapo badala ya kutatua migogoro isiyokuwa na maana. Pia ameshauri wanachuo kusikiliza sera za wagombea kwa umakini mkubwa ili kuepuka KUUZIWA MBUZI KWENYE GUNIA.
 
 MSHAURI WA WANAFUNZI ALITUMIA FURSA HIYO KUWAASA WAGOMBEA KUTUNZA MAZINGIRA HASA KUTOBANDIKA MABANGO SEHEMU ZISIZO RASMI
                                         NAYE MAKAMU WA CHUO AKASEMA;
Makamu mkuu wa chuo amewatakia wanafunzi kampeni njema zenye baraka na fanaka na zinazozingatia sheria na taratibu za chuo.

Hakuna maoni: