ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 11 Mei 2015

USAJILI: Simon Msuva aiangukia Yanga

Msuva 
Na Khatimu Naheka na Iman Makongoro, 
Kwa ufupi
  • Ukiacha Nonda Shaaban ‘Papii’, hakuna mchezaji mwingine aliyefanikiwa kung’ara au kuuzwa nje ya nchi akitokea Yanga.

Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva amereja nchini akitokea Afrika Kusini kufanya majaribio ya soka la kulipwa na amewaangukia viongozi wake kutofanya makosa ya kuzuia uhamisho wake.
Msuva mfungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara, katikati ya wiki iliyopita alitoroka na kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio katika klabu ya Bidvetes Wits inayoshika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu nchini humo ikiwa na pointi 52 juu ya Mamelodi Sundowns 57 na vinara Kaizer Chiefs wenye pointi 69.
Akizungumza na gazeti hili mara baada ya kuwasili juzi, Msuva alisema amefanikiwa kuandika historia katika maisha yake ya soka kwa kufanya majaribio katika klabu ya Wits na sasa anasubiri majibu ya majaribio hayo kabla ya kuanza mchakato wa uhamisho.
Msuva ambaye amefunga mabao 17 katika Ligi Kuu msimu huu alisema anauomba uongozi wa klabu yake chini ya mwenyekiti Yusuf Manji kutoweka ugumu katika uhamisho huo badala yake wafanye taratibu nyepesi ili aweze kucheza soka nje ya Tanzania.
“Unajua haya ni maisha na hii ni nafasi yangu ya pekee niliyopata, nashukuru kila kitu kilienda sawa, ombi langu kwa uongozi ni kunisaidia nikamilishe ndoto yangu,”alisema Msuva.
“Uongozi ningeuomba endapo hawa jamaa (Wits) watakuja kuanza mchakato wa usajili wasiwe na tamaa ya fedha kwa kutaja kiasi kikubwa ambacho kitakwamisha uhamisho wangu.”
Katibu Mkuu wa Yanga, Jonas Tiboroha alilithibitishia gazeti hili jana kuwa  hawana mpango wa kumuwekea vikwazo Msuva huku akibainisha kuwa wanachohitaji ni taratibu zifuatwe ingawa hadi jana mchana hakuna kiongozi wala wakala wa klabu ya Bidvest aliyewafuata.
“Kama kweli wana nia na Msuva, tuko tayari kumwachia akatafute maisha mengine ya soka nje ya nchi, madai kuwa tuna mpango wa kuweka dau kubwa ili kumkomoa si kweli, tutaweka dau ambalo kwetu tunaona ndilo linafaa kumuuza Msuva,” alisema katibu huyo.
“Kama timu inayomtaka itashindwa dau letu basi haimuhitaji, mbona kuna wachezaji wanauzwa hadi dola milioni moja, dola laki saba na kuendelea? Hivyo Msuva ‘akithitibisha’ anaweza, fedha tunayoitaka haitakuwa ya kushtua,” alisema Tiboroha bila kubainisha ni kiasi gani.
Tiboroha alisema walitarajia kukutana na Msuva jana jioni ili kujua hatma yake endapo anaondoka Yanga au la.
Yanga imekuwa na tabia ya kuwazuia wachezaji wake wanapotakiwa na klabu mbalimbali nje ya nchi, ilishafanya hivyo kwa Jerryson Tegete na Mrisho Ngassa na Haruna Niyonzima.
Mwaka 2009, Ngassa alitakiwa bila ya kufanya majaribio katika  klabu ya Lov-Ham ya Norway kwa gharama ya Dola za Marekani 50,000, lakini Yanga walisema klabu yao ni kubwa ambayo haina shida na ina uwezo wa kuwalea wachezaji wake na ndiyo maana haipo tayari kuwauza nyota wake kwa bei rahisi na pengine wangelipwa zaidi ya Dola za Marekani 100,000 wangeweza kumwachia.(Mwananchi)

Hakuna maoni: