ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 21 Mei 2016

Mama aua mwanawe kwa kumuibia 8,000/-

Imeandikwa na Ahmed Makongo, Bunda
MWANAMKE mmoja anashikiliwa na polisi wilayani Bunda, mkoani Mara kwa tuhuma ya kumuua mtoto wake kwa kipigo, baada ya kumtuhumu kumuibia Sh 8,000.
Kamanda wa polisi mkoani Mara, Kamishina Msaidizi wa Polisi Ramadhan Ngazi juzi alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo, lililotokea majira ya saa 11:30 jioni katika mtaa wa majengo eneo la Bunda Day mjini hapa.
Pili Omondo (28), mkazi wa mtaa huo alimpiga kwa fimbo kichwani mtoto wake ambaye alikuwa mwanafunzi wa shule ya msingi Kabarimu na kumsababishia kifo.
Alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Wakuru Rungu (9) na kwamba baada ya kipigo hicho alimbeba na kumpeleka hospitalini, akidai kwamba amegongwa na pikipiki na ndipo muda mfupi akapoteza maisha. Kamanda Ngazi alisema kuwa mtuhumiwa huyo bado anashikiliwa na polisi na upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma ya mauaji ya mwanawe.
Habari kutoka eneo la tukio zinadai kuwa mwanamke huyo alimpiga mtoto wake kwa kumgongesha kichwa ukutani akidai ni mwizi sugu na kwamba baadhi ya majirani walipomzuia alidai kwamba hata kama akimuua ni mwanawe.
Katika tukio lingine, mwanamke mmoja ambaye hajafahamika jina wala makazi yake amejifungua kichanga na kukitupa pembezoni mwa barabara kuu ya Mwanza-Musoma, katika eneo la mtaa wa Balili mjini hapa.

MAGAZETINI:#Wanafunzi wengi zaidi vyuo vikuu kukopeshwa

Imeandikwa na Regina KumbaWANAFUNZI zaidi wa elimu ya juu, wanatarajiwa kuanza kupata neema baada ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, kuongeza makusanyo yake kuanzia mwezi ujao kutokana na kujipeleka wenyewe kwa wadaiwa wa bodi hiyo.
Neema hiyo inatarajiwa baada ya bodi hiyo kupokea mwitikio mkubwa wa wadaiwa wa mikopo, kuanzia mwezi Juni wanatarajia kuanza kukusanya Sh bilioni nane kwa mwezi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo wa bodi hiyo, Robert Kibona alisema ongezeko hilo la fedha litasaidi kukopesha wanafunzi wengi zaidi, ambao awali walikuwa wakiachwa kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha.
Alisema baada ya kufanikiwa kongeza idadi ya wadaiwa na bodi, wanatarajia kuongeza makusanyo ya fedha ambayo ni Sh bilioni nane kwa mwezi kuanzia mwezi Juni mwaka huu ikilinganishwa na hapo nyuma walipokuwa wakikusanya Sh bilioni 2.7 tu.
“Fedha hizo tutakazokusanya zitatusaidia sasa kukopesha wale ambao walikuwa wanakosa mkopo, kazi yetu sisi ni kukusanya fedha na kukopesha,” alisema Kibona.
Hii itakuwa msaada mkubwa hasa ikizingatiwa kumekuwa na malalamiko mengi ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kutopata fedha za mikopo kwa wakati na wengine kukosa kabisa ingawa fani wanazosomea zinafaa kupewa mkopo.
Kibona alisema mwitikio huo wa watu kujitokeza kuanza kulipa mikopo yao, ni baada ya bodi kutoa notisi ya siku 60 tangu Machi 14 mwaka huu kwa wanufaika wote wa mikopo wanaodaiwa kujitokeza na kuanza kulipa madeni yao kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kibona alisema siku hizo 60 zilikamilika Mei 13 mwaka huu na katika muda huo, waajiri pia walitakiwa kuhakikisha wanawasilisha taarifa za waajiri wao waliohitimu katika vyuo vya elimu ya juu ndani ya nchi.
“Lengo la tangazo hilo ilikuwa ni kuhakikisha madeni yanakusanywa ili kuongeza uwezo wa kukopesha watanzania wengi zaidi, hivyo tulipata jumla ya wanufaika wa mikopo 21,721 ambao wanadaiwa Sh bilioni 151.5,” alisema Kibona.
Aidha Kibona alisema katika kipindi hicho cha siku 60 wanufaika 2,007 ambao wanadaiwa jumla ya Sh bilioni 1.93 waliwasiliana na Bodi ya Mikopo kwa kwenda ofisini au kwa barua ili kuanza kurejesha mikopo yao.
Alisema katika siku hizo 30 zilizoongezwa ambazo zilianza jana na zitaisha Juni 20 mwaka huu, Bodi inatoa mwito kwa wanufaika wote, wadhamini au wazazi pamoja na waajiri waliobaki kujitokeza kwani baada ya hapo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Magazeti ya Leo jumamosi ya tarehe 21 may 2016























Alhamisi, 19 Mei 2016

MAGAZETINI:#Cannavaro aitwa Stars, Kabunda, Mgunda ndani

Imeandikwa na Rahel Pallangyo
KOCHA Mkuu wa timu ya Soka ya Tanzania, Charles Boniface Mkwasa ameita kikosi cha wachezaji 27, akiwemo nahodha wa zamani wa timu hiyo aliyetangaza kustaafu, Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Pia katika kikosi hicho ameita winga chipukizi Hassan Kabunda wa Mwadui FC ya Shinyanga, ambaye ni mtoto wa beki wa zamani wa Yanga, Salum Kabunda ‘Ninja’ (sasa marehemu).
Mkwasa pia amemjumuisha mshambuliaji Jeremiah Juma wa Prisons ambaye ni mtoto wa mshambuliaji wa zamani wa Coastal Union, Juma Mgunda.
Kikosi hicho kinajiandaa kucheza Misri Juni 4, 2016 katika mchezo wa kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2017), ambapo kabla ya kuivaa Misri itacheza mechi ya kirafiki na timu ya Taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’ mwishoni mwa mwezi huu.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkwasa amesema amemjumuisha Cannavaro kwani baada ya kupona ameonesha kiwango kikubwa na kusema hajawahi kupata barua yoyote kutoka kwake inayomtambulisha kuwa amestaafu kuichezea timu hiyo.
Cannavaro kwa nyakati tofauti alinukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari kuwa amestaafu kuchezea timu hiyo, baada ya Mkwasa kumtangaza Mbwana Samata kuwa nahodha wa Taifa Stars. Alisema amemuita Cannavaro na kumuacha beki wa Yanga, Kelvin Yondani anayetumikia adhabu ya kadi mbili za njano.
Kikosi kamili na timu zao katika mabano ni Deogratius Munishi (Yanga), Aishi Manula (Azam FC) na Benny Kakolanya (Tanzania Prisons) wakati mabeki ni Horoub, Mwinyi Haji na Juma Abdul (Yanga), Aggrey Morris, David Mwantika na Erasto Nyoni (Azam FC), Mohammed Hussein (Simba) na Vincent Andrew (Mtibwa Sugar).
Viungo ni Himid Mao, Farid Mussa (Azam), Jonas Mkude na Mwinyi Kazimoto (Simba), Mohammed Ibrahim na Shiza Kichuya (Mtibwa Sugar), Ismail Issa (JKT Ruvu), Juma Mahadhi (Coastal Union) na Hassan Kabunda (Mwadui FC) Washambuliaji ni Thomas Ulimwengu (TP Mazembe), Mbwana Samatta (KRC Genk), Elias Maguli (Stand United), Ibrahim Ajib (Simba), John Bocco (Azam), Deus Kaseke (Yanga) na Jeremiah Juma (Tanzania Prisons).

Ni Yanga ya kimataifa



Imeandikwa na Mwandishi Wetu

YANGA inaleta heshima kwa Watanzania. Pengine ndivyo unavyoweza kuzungumzia matokeo ya mchezo wa Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF CC), ambapo Yanga imeingia hatua ya makundi ya mashindano hayo.
Imevuka licha ya kufungwa 1-0 na wenyeji wao, Sagrada Esperanca ya Angola katika mchezo uliofanyika katika mji wa Dundo.
Bao pekee la Waangola hao liliwekwa kimiani na mshambuliaji mkongwe mwenye umri wa miaka 37, lakini mahiri, Arsenio Sebastiao Cabungula `Love’ katika kipindi cha kwanza.
Yanga imenufaika na ushindi wa 2-0 ilioupata Mei 7 jijini Dar es Salaam kutokana na mabao ya Simon Msuva na Matheo Anthony, na hivyo kufuzu kwa jumla ya mabao 2-1.
Katika mchezo wa jana, Yanga ilicheza kwa nguvu zaidi karibu muda mwingi wa mchezo, ambapo washambuliaji wake wakiongozwa na Donald Ngoma walifika mara kadhaa langoni mwa wapinzani wao, lakini umaliziaji ulikuwa mbaya.
Dakika ya 90, kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ alipangua penalti iliyotolewa baada ya beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kumchezea madhambi mshambuliaji wa Sagrada.
Kwa kuingia hatua ya makundi Yanga imeandika historia mpya katika soka nchini kwa kuwa klabu ya kwanza Tanzania kufuzu hatua hiyo katika mashindano hayo, lakini ni mara ya pili kufuzu hatua ya makundi kwa mashindano makubwa Afrika baada ya kufanya hivyo mwaka 1998 katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Simba ya Dar es Salaam nayo ilifuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka 2003 kwa kuitoa na kuivua ubingwa Zamalek ya Misri. Yanga imeangukia Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF CC), baada ya kutolewa na Al Ahly ya Misri hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 3-2, ililazimishwa sare ya 1-1 Dar es Salaam na kufungwa mabao 2-1 Alexandria, Misri.
Ilizitoa Cercle de Joachim ya Mauritius kwa mabao 3-0, ikishinda 1-0 ugenini na 2-0 nyumbani kabla ya kuitoa APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2, ikishinda 2-1 Kigali na kutoa sare ya 1-1 Dar es Salaam.
Kwa upande wao, Sagrada Esperanca katika Raundi ya Awali waliitoa Ajax Cape Town ya Afrika Kusini kwa mabao 3-2 baada ya kufungwa 2-1 ugenini na kushinda 2-0 nyumbani.
Katika raundi ya kwanza waliitoa LD Maputo ya Msumbiji kwa mabao 2-1, ikishinda 1-0 nyumbani na kutoa sare ya 1-1 ugenini na kwenda hatua ya 16 Bora, ambako waliitoa V.Club Mokanda ya Kongo kwa jumla ya mabao 4-1 wakishinda 2-1 ugenini na 2-0 nyumbani.
Pamoja na Yanga katika hatua hii, timu nyingine zilizoingia na zimeshaanza kucheza mechi za mtoano – mbili, nyumbani na ugenini kabla ya nne kufuzu kwa hatua ya makundi zikichanganywa na zilizokuwamo ni Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini na Al-Merreikh ya Sudan.
Nyingine ni TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC); Etoile du Sahel ya Tunisia; Stade Malien ya Mali; Al-Ahli Tripoli ya Libya; MO Bejaia ya Algeria.
Kutokana na kusonga mbele huko na kuingia katika makundi, kama Yanga ikishika nafasi ya nne itavuna dola 150,000 (Sh milioni 315) huku Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakilamba dola 15,000 (Sh milioni 31.5).
Wakishika nafasi ya tatu kwenye kundi wanachukua dola 239,000 (sh milioni 501) na TFF kupata dola 20,000 (Sh milioni 42).
Yanga hawa ambao kocha msaidizi ni Juma Mwambusi waliyemchukua Mbeya City baada ya Charles Boniface Mkwasa ‘Master’ kwenda Taifa Stars wakishika nafasi ya pili kwenye kundi lao watapata dola 239,000 na shirikisho la Rais Jamal Malinzi yaani TFF linapata dola 25,000 (Sh milioni 52.5).
Yanga wakifika fainali; hata wasipolitwaa kombe basi watakuwa tayari mezani mwao wana dola 432,000 (Karibu Sh milioni 900) na TFF kupata dola 30,000 (Sh milioni 62) na ikiwa wanafunika bara zima kama Mlima Kilimanjaro ulivyo paa la Afrika, zao ni dola 625,000 (zaidi ya Sh bilioni 1.3 za Tanzania) na TFF wanalamba dola 35,000 (zaidi ya Sh milioni 70).
Yanga; Deo Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Vincent Bossou, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Mbuyu Twite, Simon Msuva, Thabani Kamusoko/ Deus Kaseke, Donald Ngoma, Amissi Tambwe/Kevin Yondan na Haruna Niyonzima.

                                                               TANGAZO 
                            NEW  MWALIMU EDUCATION CENTRE
Mahali: Ilula madizini katika majengo ya kanisa katoriki kigango cha madizini karibu na soko la TASAF.
Inawatangazia kuwa inaendelea na utoaji wa huduma (tuition) kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita: tuition hii ni mahususi kwaajili ya likizo ya mwezi wa sita itaanza usajiri wake kuanzia tarehe 30/05/2016.
Ada ni shilingi Elfu kumi(10,000) kwa muda wote wa likizo
- kwa wanafunzi wa kidato cha nne(form 4) tutafanya solving ya past paper na maswali mbalimbali
pia mwanafunzi atapewa peni bure na notes zilizo andaliwa na walimu mahili mara tu baada ya kufanya usajiri. Nyote mnakaribisha kwa mawasiliano piga simu no +255769694963 au +255784428256.