Waziri wa TAMISEMI amesema ajira mpya za walimu mwaka huu zitatoka pale bajeti hiyo itakapopitishwa ili kuepuka usumbufu ameyasema hayo alipokuwa katika mahojiano na clouds tv leo tar 30/03/2016
ALIYEKUWA Spika wa Baraza la Wawakilishi kwa zaidi ya miaka 20 sasa,
Pandu Ameir Kificho, ameng’olewa katika nafasi hiyo baada ya kushindwa
katika kura za kuwania awamu nyingine ya uongozi wa baraza hilo.
Badala yake wajumbe wateule wa Baraza la Wawakilishi, wamemchagua
Zubeir Ali Maulid, kuwa Spika mteule wa baraza hilo, baada ya kupata
kura 55 na kumuacha kwa mbali Kificho aliyeambulia kura 11 katika
uchaguzi uliofanyika jana katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar.
Aidha katika uchaguzi huo ambao wawakilishi 72 walipiga kura, Janeth
Nora Sekihola ambaye ni hakimu mstaafu akipata kura 4 wakati kura mbili
ziliharibika.
Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuangushwa
katika uchaguzi huo, Kificho alisema amekubali kushindwa na yupo tayari
kutoa ushirikiano akitakiwa kufanya hivyo.
“Hiyo ndiyo demokrasia, nimekubali kushindwa na nipo tayari kutoa
ushirikiano mkubwa nikitakiwa kufanya hivyo kwa sababu ni ukweli kwamba
ninao uzoefu mkubwa katika nafasi hiyo kwa zaidi ya miaka 20,” alisema.
Naye Spika mteule wa baraza hilo, Maulid alisema anakabiliwa na
changamoto kubwa ya kuleta maendeleo na mabadiliko makubwa katika chombo
hicho ambacho ni moja ya mihimili ya dola katika utekelezaji wa
majukumu yake.
Amesema atatumia uzoefu alioupata kufanya kazi katika taasisi za
kutunga sheria, kwa ajili ya kuleta mabadiliko hayo kwa kuhakikisha
kwamba Baraza la Wawakilishi linafanya kazi inayotakiwa ya kuisimamia
Serikali kwa mujibu wa Katiba.
“Nimekuwa Mwakilishi Shauri Moyo na Waziri mwaka 2000, pia nimekuwa
Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa miaka miwili na nusu kwa
hivyo uwezo wa kufanya kazi katika mabunge ya Jumuiya ya Madola ninao
mkubwa,” alisema.
Aliwaomba wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wateule kumpa kila aina ya
ushirikiano utakaomwezesha kutekeleza na kutimiza majukumu yake kwa
mujibu wa Katiba, kwani chombo hicho ni moja ya mihimili ya dola.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliozungumza na gazeti
hili, wamesema kwamba mabadiliko hayo ni ishara na ujumbe tosha kwa Rais
wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kwamba wawakilishi wanataka
mabadiliko makubwa kwa Serikali kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
“Mabadiliko makubwa tuliyoyafanya sisi wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi kwa kumchagua Zubeir Ali Maulidi kuwa Spika mteule mpya, ni
dalili tosha kwamba sasa tunataka mabadiliko makubwa ndani ya Serikali
kwa kuwa na viongozi watakaowatumikia wananchi moja kwa moja,” alisema
Rashid Ali Juma mwakilishi mteule wa jimbo la Amani.
Kificho ameweka historia kuwa Spika wa Kwanza katika Baraza la
Wawakilishi la mfumo wa vyama vingi kuanzia mwaka 1995, ambapo kabla ya
kuchaguliwa kushika wadhifa huo, alikuwa mwakilishi wa Jimbo la
Makunduchi kuanzia 1988.
Zubeir Ali Maulid mwaka 2000 alichaguliwa kuwa Mwakilishi wa Shauri
Moyo kwa tiketi ya CCM na kuteuliwa kuwa Waziri wa Mawasiliano na
Uchukuzi, chini ya Serikali ya Rais mstaafu Amani Abeid Karume, ambapo
alidumu katika wadhifa huo kwa miaka mitatu.
Mwaka 2005, Zubeir alichaguliwa kuwa Mbunge wa Kwamtipura kwa tiketi
ya CCM ambapo akiwa bungeni katika kipindi cha miaka miwili na nusu,
alikuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na kuongoza vikao
mbali mbali kwa kusaidiana na spika na naibu spika.
Katika hatua nyingine, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein, amemteua Said Hassan Said, kuwa
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Uteuzi huo
ndio wa kwanza kufanyika, tangu Rais Shein alipokula kiapo cha kuongoza
Zanzibar kwa miaka mitano ijayo Alhamisi ya wiki hii.
UCHAGUZI
wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam ambao unaendele kufanyika muda huu
katika ukumbi wa Kareemjee taarifa za ndani kutoka katika uchaguzi huo
zimeeleza kuwa mgombea wa vyama vya UKAWA, kupitia chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema), Mh. Isaya
Mwita ameibuka kidedea kwa kupata kura 84 huku CCM wao wakipata kura 67
na kati ya jumla ya kura hizo 7 ziliaribikaambapo jumla ya kura za
wajumbe wote ni 158.
Hali
ilivyo muda huu ndani ya uchaguzi huo wa Umeya wa Jiji la Dar es Salaam
muda huu leo Machi 22.2016, ambapo UKAWA wameibuka kidedea
Mhe.
Issaya Mwita (mbele) ambaye hadi sasa vyanzo vya ndani kutoka uchaguzi
huo ameweza kupata kura 84 dhidi ya mshindani wake kutoka CCM ambaye
alipata kura 67 huku kura 7 zikiharibika, hivyo kuibuka na ushindi wa
Umeya wa Jiji. (Picha ya Maktaba).
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, George Simbachawene ametangaza leo
March 21, 2016 kuwashughulikia wale wote wanaofanya hujuma katika sekta
ya elimu nchini, wakiwemo Walimu wanaokimbia sehemu zao za kazi hususani
vijijini na kukimbilia mijini.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari leo March 21, 2016 alisema…‘Katika
eneo la upangaji waWalimu ni tatizo kubwa na nadiliki kusema hadharani
kwamba upangaji wa walimu kwenye shule zetu ni wa ovyo leo hii
tunaupungufu wa ualimu kwenye vijiji kwa asilimia zaidi ya 40% na
ongezeko la walimu mijini ni kama asilimia 50% kwa maana ya kwamba
walimu wengi wapo Dar es Salaam, walimu wengi wapo kwenye miji mikubwa
makao makuu ya mikoa na makao makuu ya wilaya’ – George Simbachawene
‘Hata
wanawake wanasema wanafuata wanaume zao huko ni kukosa uzalendo kama
ulikubali kuajiliwa lazima ukubali kufanya kazi mahala popote pale na
watanzania ni wote mpaka waliopo kule vijijini haiwezekani kukubali kazi
mjini na kukataa kijijini’ – George Simbachawene
kwa tafsiri hii ya waziri wa TAMISEM hakutokuwa na sababu zzisizona msingi zitakazokubalika kwa walimu wapya kwa mwaka 2016
MBUNGE
wa jimbo la Kilolo Venance Mwamoto ameahidi kuongozana na wazee
wa mji wa Ilula kwenda Dodoma kuonana na waziri mkuu Kassim
Majaliwa ili kumfikishia ahadi ya maji ya Rais Dr John Magufuli kwa
wananchi wa mji mdogo wa Ilula .
Huku
akiwataka wananchi wa Ilula na Nyalumbu kutomchagua mwaka 2020 iwapo
atashindwa kutekeleza ahadi ya maji katika mji huo wa Ilula ndani ya
miaka yake mitano ya ubunge.
Akizungumza
na wananchi wa kata ya Nyalumbu na Ilula wakati wa mikutano yake
ya hadhara ya kuwashukuru wananchi wake kwa kumchagua kuwa mbunge
wa jimbo hilo la Kilolo jana ,Mwamoto alisema kuwa kero ya maji
katika mji wa Ilula imekuwa ya muda murefu jambo ambalo hatataka
kuona wananchi hao wakiendelea kutabika.
Alisema
kuwa kero hiyo ya maji imeanza kuwasumbua wananchi hao toka nchi
ipate uhuru wake mwaka 1961 hadi leo wapo katika mahangaiko ya maji
na baadhi ya viongozi wameendelea kufanya udanganyifu wa mradi huo
kama ambavyo mwaka 2010 viongozi walivyomdanganya aliyekuwa
makamu wa Rais Dr Alli Mohamed Shein kwa kupelekwa kufungua mradi
wa maji ambao viongozi walimdanganya kwa kujaza maji katika tanki
hilo ili azindue mradi huo.
Hivyo
alisema udanganyifu huo hautapewa nafasi katika uongozi wake wa
miaka mitano lazima kero hiyo imalizike na wananchi hao waweze
kupata maji vinginevyo yupo tayari kuongoza wananchi wake kumzuia
waziri wa maji kupita Ilula kwenda jimboni kwake Njombe iwapo wananchi
hao hawatatimiziwa ahadi yao ya maji safi na salama .
Mbunge
huyo alisema katika kikao kijacho cha bunge kinachoanza mwezi ujao
ataomba wananchi wa Ilula na Nyalumbu kumteulia wazee watatu ama
wanne ili kwenda nao bungeni Dodoma kukutana na waziri mkuu ili
kwa ajili ya kumkumbusha ahadi ya Rais ya maji katika mji huo wa Ilula
.
Pia
aliagiza mamlaka ya maji ya mji mdogo wa Ilula kuchunguza vema mradi
wa maji uliopo kama umejengwa kwa kiwango ama chini ya kiwango maana
amesema mradi mdogo uliopo kwa sasa bado umekuwa na kero kubwa ikiwa
ni pamoja na baadhi ya maeneo kuvujisha maji huku akiwataka wananchi
kwa upande wao kutunza miundombinu ya maji.
Mbunge wa Kilolo Bw Venance Mwamoto (kushoto) akisalimiana na mmoja kati ya wazee wa mji wa Ilula aliyetoka kuchota maji
Katika
hatua nyingine mbunge Mwamoto alimshauri meneja wa maji wa IRUWASA
katika mji wa Ilula Teodolah Mvungi kuangalia uwezekano wa kuboresha
kituo cha maji eneo la Ilula ili kiweze kunufaisha wananchi wengi
na kuwa iwapo wataanza uboreshaji kwa upande wake ataunga mkono .
Wananchi
wa Zanzibar leo wanapiga kura katika uchanguzi wa marudio baada ya
kufutwa kwa uchanguzi uliofanyika October 25,2025 kutokana na kasoro
zilizojitokeza.
Katika baadhi ya vituo wananchi wamejitokeza na zoezi linaendelea vizuri huku hali ya usalama ikiwa imeimarishwa.
Katika kituo cha shule ya sekondari Muembeladu ambayo ina vituo sita,vituo vitano vinawatu 350 na kituo kimoja kina watu 91. Akizungumza na wanahabari, msimamizi wa kituo hicho amesema zoezi la upigaji kura linaendelea vizuri katika jimbo la Jangombe .
Kwa
upande wa kituo cha skuli ya Muembeshauri nako hali ni shwari na zoezi
linaendelea vizuri ambapo katika skul hiyo vituo 11 vinatumika watu
kupiga kura.
Katika Jimbo la kikwajuni, zoezi linaendelea vizuri huku mwitikio wa watu ukiwa ni mkubwa.
Baadhi
ya wananchi waliojitokeza kupiga kura wamesema zoezi hilo limekua
rahisi na la amani tofauti na taarifa zilivyokua zinasambazwa.
Mkazi
wa Muembeshauri aliyejitambulisha kwa jina la Hamidu Salum Haji ametoa
wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kwani zoezi la kupiga kura
linaendelea kwa amani na utulivu.
“Ndugu zangu tusikubali kugombanishwa na watu ambao hawaitakii mema Zanzibar tusimame pamoja katika kutetea nchi yetu” amesema Haji
Wakati zoezi hilo linaendelea maduka mengi yamefunguliwa na wafanyabiashara wanaendelea na kazi kama kawaida
Rais wa Zanzibara na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Ali Mohammed Shein leo amepiga kura katika kituo cha skuli ya bungi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, amepiga kura katika kituo cha skuli ya Kiembe samaki
Mgombea
urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar Dkt Ali Mohammed
alizungumza na wanahabari baada ya kupiga kura yake katika kituo cha
Bungi, Kibera kisiwani Unguja ambapo alisema anaamini atashinda kwa
kishindo na kuhusu kushindwa alisema tusubiri matokeo ya uchaguzi ndiyo
yataamua.
"Nimepata
nafasi ya kupiga kura kama haki yangu ya kimsingi na kumekuwa na
utulivu mkubwa kwenye zoezi hili,hali ya ulinzi imeimarishwa.
"Matumaini yangu ni kushinda kwa kishindo, kuhusu kushindwa ndugu muandishi tusubiri matokeo ndiyo yataamua".Alisema Dkt. Ali Mohammed Shein
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd amepiga kura katika kituo cha skuli ya Kitope
DAKTARI Vicent Mashinji ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kupitishwa na Baraza Kuu
la Chadema, katika kikao chake kilichokaa jijini Mwanza, anaandika Mwandishi Wetu.
Katika Kikao hicho cha Baraza Kuu, Freeman Mbowe
alitangaza jina la Dk. Mashinji na kuungwa mkono na wajumbe wa baraza
hilo, hivyo anajaza nafasi iliyoachwa na Dk. Willibrod Slaa,
aliyejienguwa ukatibu mkuu wa chama hicho.
Jina la Dk. Machinji halikuwa miongoni mwa wanachama wa Chadema ambao
walikuwa wanatarajiwa kumrithi Dk. Slaa kwani waliokuwa wanatabiriwa
kukatia kiti hicho ni Salum Ally Mwalimu, Frederick Sumaye, Benson
Kigaila, John Mnyika, Dk. Marcus Albanie na Prof. Mwesiga Baregu.
Nafasi ya Katibu wa Chadema ilikuwa wazi tangu Dk. Slaa alipoondoka
Chadema muda mfupi baada ya chama hicho kumpitisha Edward Lowassa
aliyetokea CCM kuwa mgombea urais wa chama hicho na kuungwa mkono na
vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). Wasifu wa Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Vincent B. Mashinji Professional experience
Clinical Advisor & TB/HIV lead
UMSOM-IHV
July 2008 – Present
ART Program Doctor/IMA team lead
IMA Worldhealth
August 2006 – June 2008 (1 year 10 months)
Medical Officer/Anaesthesiology
Regency Medical Centre
October 2005 – August 2006 (10 months)
Medical Officer
Muhimbili National Hospital
August 2003 – October 2005 (2 years 2 months)
Research Assistant
Freelance
November 2002 – August 2003 (9 months)
Intern Docor
Muhimbili National Hospital
September 2001 – October 2002 (1 year 1 month) Education history
Open University of Tanzania
PhD
August 2010 – Present
AMREF/UCLA Anderson School
MDI Certificate
April 2010 – April 2010
Blekinge Institute of Technology
MBA
September 2007 – March 2010 (2 years 6 months)
UMSOM-IHV
IPEP Certificate
May 2008 – May 2008
Evin School of Management
Certificate in CSR
October 2005 – October 2005
Muhimbili University College of Health Sciences
MMed/Anaesthesiology
September 2003 – April 2005 (1 year 7 months)
Muhimbili University College of Health Sciences
Certificate in Research Methodology
September 2004 – September 2004
Makerere University
MBChB
October 1995 – July 2001 (5 years 9 months)
Mzumbe High School
ACSEE
July 1992 – June 1994 (1 year 11 months)
St. Pius X Seminary, Makoko
GCSEE
January 1988 – October 1991 (3 years 9 months)
Iligamba Primary School
Leaving Certificate/Primary School
January 1981 – October 1987 (6 years 9 months
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao
13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa
vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa
Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.
Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu wa Mkoa wa Geita.
Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
Mh. Anna Malecela Kilango - Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Mhandisi Methew Mtigumwe - Mkuu wa Mkoa wa Singida.
Mh. Antony Mataka - Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
Mh. Aggrey Mwanri - Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
Mh. Martine Shigela - Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Mh. Jordan Mungire Rugimbana - Mkuu wa Mkoa Dodoma.
Mh. Said Meck Sadick - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
Mh. Magesa Mulongo - Mkuu wa Mkoa Mara.
Mh. Amos Gabriel Makalla - Mkuu wa Mkoa Mbeya.
Mh. John Vianey Mongella - Mkuu wa Mkoa Mwanza.
Mh. Daudi Felix Ntibenda - Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Mh. Amina Juma Masenza - Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
Mh. Joel Nkaya Bendera - Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
Mh. Halima Omary Dendegu - Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
Dkt. Rehema Nchimbi - Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
Mhandisi Evarist Ndikilo - Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
Mh. Said Thabit Mwambungu - Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
Luteni Mstaafu Chiku Galawa - Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).
Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman
Mbowe, yupo katika wakati mgumu kutokana na wajumbe wa Baraza Kuu na
wabunge wenye ushawishi kumtaka amteue Waziri Mkuu wa zamani, Frederick
Sumaye, kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho.
Hii inakuwa mara ya kwanza kutokea katika historia ya kuasisiwa kwa
chama hicho kikuu cha upinzani kwa wajumbe wa Baraza Kuu kumshawishi
Mwenyekiti kumteua mtu anayefaa kushika wadhifa huo.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu, linalotarajiwa kuketi leo wanaotajwa
kujipanga kumshawishi Mwenyekiti kumteua Sumaye kuwa Katibu Mkuu ni
Profesa Mwesiga Baregu, Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu na
Mbunge wa Iringa, Mchungaji Peter Msigwa.
Wengine ni pamoja na Makamu Mwenyekiti Bara, Profesa Abdallah Safari,
Makamu Mwenyekiti Zanzibar, Said Issa, Anthony Komu na Benson Kigaila
na Katibu Mkuu Baraza la Wanawake (Bawacha), Grace Tendega.
Katika orodha hiyo pia wamo wabunge wenye ushawishi mkubwa ambao ni
Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Mbunge wa
Ukonga, Mwita Waitara.
Katika orodha hiyo yumo Mbunge wa zamani wa Ilemela, Ezekia Wenje na
baadhi ya waliokuwa wagombea ubunge wenye ushawishi mkubwa ndani ya
chama.
Hadi jana Profesa Safari hakuwa amehudhuria vikao vya Mwanza kutokana na kile kilichoelezwa kukabiliwa na matatizo mbalimbali.
Juzi Lissu aliweka wazi sifa za kiongozi aliyekuwa akimtaka, jambo
ambalo lilitafsiriwa na wachambuzi wa mambo kwamba alikuwa akimuelezea
Sumaye.
Naye mmoja wa wajumbe ambaye hakupenda jina lake litajwe anayemuunga
mkono Sumaye ashike nafasi ya Katibu Mkuu, alisema ukiondoa sifa
alizotaja Lissu za kumtaka Katibu Mkuu anayeweza kuzungumza na
Watanzania, vyama vya Ukawa, ndani na nje ya nchi wakamsikiliza,
nyingine ni mtu aliyeingia Chadema kwa kutofuata cheo.
“Hakuna mwingine zaidi ya Sumaye, ambaye alijiunga na chama hiki
wakati ambao nafasi nyingi zilikuwa zimeshanyakuliwa na wanachama
wengine,” alisema mjumbe huyo.
Sababu kubwa ya wajumbe kumtaka Sumaye inaelezwa kutokana na kubaini
kuwepo kwa mpango wa Mwenyekiti, Mbowe kumtaka Salum Mwalimu, anayekaimu
nafasi hiyo.
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji, Gerson Lwenge amewasimamisha kazi
kupisha uchunguzi vigogo tisa wa Kampuni ya Maji Safi na Taka (Dawasco)
na kutaka aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Jackson Midala
kusakwa na kuchunguzwa na ikibainika alihusika kwenye ubadhirifu wa
maji, afikishwe mahakamani.
Kadhalika,Waziri Lwenge ameitaka Bodi ya Dawasco, kuchunguza tuhuma
za wizi wa maji zinazofanywa na baadhi ya watendaji wa kampuni hiyo kwa
kuwaunganishia maji bure kampuni na viwanda kadhaa jijini Dar es Salaam
na kulipwa ujira kila mwisho wa mwezi na viwanda hivyo.
Waziri Lwenge alitoa maagizo hayo jana jijini Dar es Salaam wakati
alipotembelea Dawasco kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe, kuona
utendaji wao na kuzungumza na watumishi hao.
Pia ameitaka bodi hiyo kuchunguza Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) na
kampuni nyingine pamoja na viwanda jijini Dar es Salaam kama wana
akaunti za maji ya Dawasco na kwamba madai ya kuwa wao wana visima vyao
vya maji, lazima ukweli upatikane.
Alisema kama kampuni inasema ina visima vyake binafsi vya maji, ni
lazima wawe na kibali walichopata kutoka Wizara ya Maji, kinachowaruhusu
wao kuchimba na kinaonesha kiwango cha maji, na kwamba kuna madai mengi
ya kampuni na viwanda kuwa na visima vyao, ila wizara haifahamu.
“Kama unadai una kisima cha maji cha kwako kibali kinatolewa na
wizara yangu, sasa yapo madai mengi viwanda vinasema vinatumia maji yao,
ila zipo taarifa kwamba wanajificha kwenye hilo na ukweli ni kwamba
wanaiba maji ya Dawasco, sasa lazima mchunguze hayo,” alisema Lwenge.
Waliosimamishwa kazi ni Meneja Rasilimali Watu, Mvano Mandawa, Meneja
Ufuatiliaji na Tathmini, Reinary Kapera, Teresia Mlengu, Emmanuel
Guluba, Peter Chacha, Fred Mapunda, Reginald Kessy, Jumanne Ngelela na
Bernard Nkenda.
“Sehemu kubwa ya upotevu wa maji ni wizi unaofanywa na wezi ambao ni
baadhi ya viwanda na kampuni kubwa kwa kushirikiana na watendaji wa
Dawasco, tuna taarifa na kila mwisho wa mwezi wako kwenye ‘payroll’
wanaenda kuchukua malipo, hawa ni majipu lazima yatumbuliwe,” alisema
Waziri Lwenge.
Mara baada ya kusomewa taarifa fupi ya utendaji kazi wa Kampuni hiyo
kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco, Cyprian Luhemeja, Waziri
Lwenge alitoa maagizo hayo na kusema pamoja na Kampuni kuwa na malengo
mazuri, lakini ni lazima ifanyiwe mabadiliko ili kupata watendaji
waadilifu.
Alisema upotevu wa maji hivi sasa ni asilimia 47 na kwamba maji hayo
yanapotea katika mazingira tatanishi na kuikosesha kampuni hiyo mapato.
Strabag Alitoa mfano mzuri wa Kampuni ya Ujenzi wa Barabara ya Strabag,
ambayo ilipewa zabuni ya kujenga barabara za mradi wa Mabasi Yaendayo
Haraka (Dart), kwamba tangu kampuni hiyo ianze kufanya kazi hadi sasa,
haijalipa Dawasco bili ya maji iliyotumia.
“Strabag walifanya wizi wa maji, wamejenga barabara lakini hakuna
malipo yoyote waliyofanyika Dawasco, wanadaiwa zaidi ya Sh bilioni 2.9
pamoja na faini na natoa siku 14, wawe wamelipa vinginevyo wakamatwe
wafikishwe mahakamani.
Waziri Lwenge alisema Serikali haiwezi kufanya kazi na wabadhirifu
ambao wako ndani ya taasisi, kampuni au mashirika yake na kusisitiza
kuwa ni lazima watendaji wasio waaminifu waondolewe ili kuleta ufanisi
nchini.
“Tunafanya mageuzi ili tufanye kazi kwa ufanisi na lazima tuwe na
watendaji waadilifu na wenye maadili, si wanaoangalia maslahi binafsi,”
alisema Lwenge. Waziri Lwenge alitoa wiki mbili kwa bodi hiyo kufanya
uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo na zile za wateja wakubwa wa Dawasco
kutokuwa na akaunti za maji, ili kuthibitisha ukweli wa madai hayo.
Maagizo mengine ni kuitaka Dawasco ifikapo Juni, mwaka huu
kuhakikisha wamefanikiwa kupunguza upotevu wa maji kwa asilimia 30 na
ifikapo 2020 upotevu huo uwe chini ya asilimia 20.
Awali Ofisa Mtendaji wa Dawasco, Luhemeja alisema changamoto kubwa ya
Dawasco ni upotevu wa maji na kubainisha katika maeneo 10 wanayohudumia
maji Dar es Salaam na Pwani, Magomeni ni eneo korofi kwa wizi wa maji.
Alisema eneo hilo hivi sasa limebainishwa na wameweka mtandao ambao
kuanzia mwisho wa mwezi huu, utabaini wezi wote lakini pia hatua
nyingine walizochukua ni kuweka vituo vya kuuza maji kwenye eneo korofi,
vinavyosimamiwa na jamii ya eneo husika.
Alisema kwa miezi kadhaa sasa, tangu kuanza kwa huduma hiyo wameweka
vituo 47 vya kuuza ambavyo vimefungiwa mita na wauzaji hutakiwa kulipa
Dawasco bili ya maji baada ya kuwauzia wateja wadogo wadogo.
Ofisa Mtendaji huyo mpya wa Dawasco, alisema kwa kipindi cha muda
mfupi tangu aingie kwenye kampuni hiyo, wamefanikiwa kuongeza mapato ya
maji kutoka Sh bilioni 2.9 mwaka jana hadi kufika Sh bilioni 7.1 Januari
mwaka huu.
Aliongeza kwamba lengo lao ifikapo Juni mwaka huu, ni kukusanya Sh
bilioni 12 kwa mwezi na hiyo ni kutokana na kuweka mifumo imara na
dhabiti ya kufuatilia mita za maji na masharti waliyopewa mameneja wa
maeneo husika ya kampuni hiyo.
Dawasco hivi sasa ina wateja waliounganishiwa mita zaidi ya 151,000
na lengo lao ni kuongeza idadi ya wateja baada ya kuongeza uzalishaji na
usambazaji wa maji hasa baada ya kuimarika kwa mitambo miwili ya maji
ya Ruvu Chini na Juu.
TIMU ya soka ya Simba na Mbeya City leo zinashuka dimbani kwenye
viwanja viwili tofauti kusaka pointi tatu muhimu katika mfululizo wa
mechi za Ligi Kuu bara. Simba itakuwa mwenyeji wa Ndanda FC kwenye
Uwanja wa Taifa Dar es Salaam wakati Mbeya City itakuwa mwenyeji wa
Stand United kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya.
Wekundu hao wa Msimbazi huenda wakapanda kileleni tena iwapo
watafanikiwa kuwafunga Ndanda Fc katika mchezo huo kwa kuwa watafikisha
pointi 51 na kuishusha Yanga yenye pointi 50.
Mwishoni mwa wiki iliyopita Simba ilikaa kileleni kwa siku mbili
kabla ya Yanga juzi kupanda na kumpiku kufuatia ushindi wake wa mabao
5-0 dhidi ya African Sports ya Tanga. Simba, Yanga na Azam FC
zinatofautiana kwa pointi chache kiasi kwamba mmoja akishinda, mwingine
anashuka.
Simba ina uwezekano wa kushinda mchezo wa Ndanda, kwani katika mchezo
wake wa raundi ya kwanza ilishinda bao 1-0 ugenini mjini Mtwara. Hali
itakuwa mbaya kwa Ndanda kama itakubali kichapo kwa mara nyingine kwani
licha ya kuwa katika nafasi ya nane, ina pointi 24 ambazo hazitoshi
kuihakikishia kubaki salama kwenye msimamo wa ligi kwa kuwa timu
zilizoko chini yake zinaweza kupanda kutokana na kutofautiana pointi
chache.
Kwa upande wa Mbeya City, huenda ikafanya vizuri leo baada ya
kuonesha kiwango bora chenye mabadiliko katika mchezo dhidi ya Simba
wiki iliyopita. Licha ya kufungwa mchezo huo, walicheza vizuri isipokuwa
inayumbushwa na ubutu wa safu yake ya ushambuliaji.
Pengine kwa vile inacheza kwenye uwanja wake wa nyumbani wanaweza
kutumia faida hiyo katika kufanya vizuri na kufuta machungu ya kufungwa
na timu hiyo ya Shinyanga bao 1-0 katika mchezo wa raundi ya kwanza.
HOMA ya pambano la raundi ya kwanza la Ligi ya Mabingwa Afrika kati
ya Yanga na APR ya Rwanda, imezidi kupanda, kiasi cha kila moja kutamba
kumshikisha adabu mpinzani wake.
Tayari makocha wa klabu hizo, Hans van der Pluijm wa Yanga na Nizar
Khanfir wa APR aliyeweka rekodi ya kuwa mwarabu wa kwanza kufundisha
soka Rwanda baada ya kuanza kazi rasmi jana, ameelezea utayari wake
kushinda mechi ya Jumamosi wiki hii huko Kigali, Rwanda.
Khanfir amekaririwa jana kuwa, ameshawaona Yanga kupitia video
mbalimbali na kwamba anataka kuwafunga Jumamosi. “Lengo letu ni kushinda
huo mchezo,”amesema na kuongeza; “Nimeona baadhi ya video zao na
tutaendelea kuwachambua katika siku chache zijazo kuelekea kwenye
mechi”.
Kwa ujumla, Khanfir amesema malengo yake makuu katika miezi sita ya
mwanzo ni kuiwezesha timu kutetea ubingwa wa Rwanda na pia kuifikisha
mbali katika Ligi ya Mabingwa Afrika. Mtaalamu huyo wa Tunisia aliongoza
mazoezi yake ya kwanza APR jana Uwanja wa Kicukiro akisaidiwa na kocha
aliyemkuta kazini, Emmanuel Rubona.
“APR ni timu kubwa Rwanda na ina heshima kubwa Afrika na pia ina
wachezaji wengi katika timu ya taifa, ambacho ndicho kilichonivutia mimi
kukubali kazi hii,” amesema Khanfir. “Wachezaji ni vijana wadogo na
timu ina uwiano mzuri ambao unafaa vizuri katika falsafa yangu.
Tunaitaka kuipeleka timu katika kiwango kingine.
Ni wajuzi na tunataka kuongeza ufundi zaidi, lakini zaidi ya hapo
nimevutiwa na timu kwa ujumla,” amesema. Wakati Khanfir akisema hayo,
Pluijm kwa upande wake amesema anatambua wanakwenda Kigali kwenye mchezo
mgumu wa ugenini dhidi ya APR, lakini watapambana wasipoteze.
“APR ni timu nzuri na watakuwa wamejiandaa vizuri, lakini sisi tuko
vizuri, tutakwenda kupambana tusipoteze mchezo, ili tumalizie vizuri
mchezo wa nyumbani,”amesema. Yanga SC inatarajiwa kuondoka leo nchini
kwenda Kigali kwa ajili ya mchezo huo, unaotarajiwa kuwa mkali na wa
kusisimua.
Mechi hiyo inatarajiwa kuchezeshwa na marefa wa Malawi Jumamosi
Uwanja wa Amahoro, Kigali Rwanda. Duncan Lengani anatarajiwa kupuliza
filimbi, wakati washika vibendera watakuwa Clemence Kanduku na Jonizio
Luwizi.
Mchezo wa marudiano wiki moja baadaye Dar es Salaam, utachezeshwa na
marefa wa Shelisheli; katikati Bernard Camille na pemebeni watakuwapo
Eldrick Adelaide na Gerard Pool.
Mchezo wa kwanza utafanyika mjini Kigali, Rwanda Machi 12 kabla ya
timu hizo kurudiana Dar es Salaam Machi 19 na mshindi wa jumla atakutana
na mshindi wa mchezo mwingine wa raundi ya kwanza, kati ya Al Ahly ya
Misri na Recreativo de Libolo ya Angola mwezi ujao.
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce
Ndalichako ameingilia kati mgogoro wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha St.
Joseph Dar es Salaam, waliogomea kufanya mitihani na kuwataka warejee
madarasani wakati matatizo yao yakishughulikiwa.
Wanafunzi hao walikuwa katika siku ya tatu ya mgomo wao jana ambapo
pamoja na mambo mengine walikuwa wakilalamikia mapungufu yaliyopo chuoni
hapo, ikiwa ni pamoja na maabara za kufanyia mafunzo kwa vitendo,
matatizo ya kiutawala, mitaala ya kufundishia pamoja na ada.
Profesa Ndalichako aliwasili chuoni hapo jana asubuhi na kukagua
mazingira ya kufundishia ya chuo hicho kwa kutembelea maabara zote
chuoni hapo na kisha kwenda kuzungumza na utawala, Serikali ya wanafunzi
na mwisho alihutubia wanafunzi wote.
Ndalichako baada ya kuzungumza na pande zote mbili aliagiza wanafunzi
hao warejee madarasani kuendelea na mitihani yao na kuutaka uongozi wa
chuo uyafanyie marekebisho mapungufu ya kiutawala yaliyojitokeza.
Aidha ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), chini ya Katibu
Mtendaji wake, Profesa Yunus Mgaya kufuatilia na kuchunguza kwa makini
madai ya wanafunzi hao juu ya kuwepo kwa wahadhiri wasio na sifa
zinazotakiwa.
RAIS John Magufuli amesema anatamani mafanikio ya nchi ya Vietnam
kiuchumi na kubainisha kuwa ziara ya Rais wa nchi hiyo, Truong Tang Sang
nchini, ni fursa na changamoto kwa watanzania kujifunza mambo mengi,
yatakayosaidia kukuza pia uchumi wa Tanzania.
Aidha amehamasisha Watanzania kuchangamkia fursa na rasilimali
zilizopo nchini katika kujiinua na kuimarisha nchi yao kiuchumi. Alisema
Tanzania ni miongoni mwa nchi tajiri kwa rasilimali na fursa nyingi,
ingawa bado iko nyuma kimaendeleo. Kwa upande wake, Rais Sang amesema
nchi yake na Tanzania zimekubaliana kushirikiana katika maeneo ya
biashara, kilimo, viwanda na uvuvi lengo likiwa ni kuhakikisha nchi zote
zinanufaika kwenye ushirikiano huo.
Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari na marais hao Ikulu
Dar es Salaam jana, Dk John Magufuli alisema ni wakati sasa wa Tanzania
kujifunza kutoka kwa nchi hiyo ya Vietnam ambayo pamoja na kukabiliwa
na vita ya muda mrefu, imefanikiwa kuwa miongoni mwa nchi zenye uchumi
wa kati. “Ukweli ni kwamba ziara ya Rais Sang nchini kwetu ni muhimu
sana na imekuja kwa wakati muafaka.
Mwaka 1976 Rais wa Vietnam alikuja nchini na alichukua mbegu ya
korosho na kuipeleka nchini kwake, na leo hii Vietnam ni moja ya nchi
zinazoongoza kwa kuzalisha korosho duniani,” alisema. Alitaja mafanikio
mengine ya nchi hiyo ni pamoja na kuwa na uchumi wa kati, licha ya
kukabiliwa na mapigano ya muda mrefu. Ilipata uhuru wake mwaka 1945 na
ilidumu kwenye mapigano hadi Julai 2, mwaka 1976.
Alisema mwaka 1977 mapato ya kila raia wake yalikuwa ni dola 100,
lakini sasa imefanikiwa kupandisha mapato hayo na sasa kila raia wa nchi
hiyo mapato yake ni dola 2000 kwa mwaka na imepunguza kiwango cha
umasikini kwa asilimia 50. “Sisi tangu mwaka 1960 bado tuko kwenye nchi
masikini, kwa hiyo hii ni changamoto kwa nchi yetu. Tunatakiwa kujifunza
kuondokana na hali hii.
Wao uzalishaji kwa mchele wanalima mara tatu kwa mwaka, sisi tunalima
mara moja tu na inawezekana uzalishaji wetu ni mdogo sana,” alisema.
Alisema nchi hiyo pamoja na kuchukua mbegu ya korosho nchini, ndio nchi
inayoongoza kwa kuzalisha korosho duniani, wakati Tanzania ndio iliyotoa
mbegu hiyo, zao hilo badala ya kuzalishwa kwa wingi ndio uzalishaji
wake unafifia.
“Samaki sina uhakika kama walichukua huku, lakini leo hii Vietnam ni
wazalishaji wa samaki wakubwa sana. Lakini kwa nchi yetu ambayo ina
maziwa 21 na mito kila mahali na bahari lakini uzalishaji wa samaki uko
chini…” “Tuna ng’ombe zaidi ya bilioni 22 hadi bilioni 23 nafikiri
tunaweza kuwa wa pili barani Afrika baada ya Ethiopia, lakini ngozi zetu
za viatu hapa tunaagiza nje.
Kwa hiyo kwa hili watanzania tunatakiwa tusiogope kujifunza kwa wale
waliotutangulia ili na sisi nchi yetu iweze kufika mahali pazuri,”
alisisitiza Dk Magufuli. Alisema ujio wa Rais Sang pamoja na ujumbe wake
wa zaidi ya mawaziri takribani 20 na wafanyabiashara ni wakati pekee wa
Watanzania na wa Vietnam, kuimarisha ushirikiano uliokuwepo kwa zaidi
ya miaka 50 sasa kuhakikisha uhusiano unaleta maendeleo kwa pande zote.
“Ziara hii ni muafaka kwetu sisi watanzania kujenga uhusiano mzuri na
nchi ya Vietnam ili kuweza kujifunza na sisi tuweze kufikia lengo letu
la kuwa nchi ya kipato cha kati,” alisema. Pamoja na hayo, Rais Magufuli
alisema katika mazungumzo yake na Rais wa Vietnam alipata mwaliko wa
kutembelea nchi hiyo mwakani. “Kwa kweli mwaliko huu nimeupokea na
ninajisikia kuthaminiwa na kuheshimiwa sana,” alisema.
Kwa upande wake, Rais Sang alisema anajisikia fahari kuona uhusiano
kati ya Tanzania na nchi yake unaimarika. Alisisitiza kuwa uhusiano na
ushirikiano huo utaleta maendeleo ya dhati baina ya nchi hizo mbili.
Alipongeza serikali kupambana dhidi ya umasikini kwa kusisitiza kuwa
inafanya vizuri kiuchumi kwani ni miongoni mwa nchi za Afrika ambazo
uchumi wake unakua kwa kasi.
“Kama rafiki wa karibu tunavutiwa na maendeleo yenu hasa katika
kupambana na umasikini lakini pia ukuaji wa kasi wa uchumi wenu. Katika
mazungumzo yetu na Rais Magufuli tumezungumzia masuala mbalimbali ya
maendeleo, ikiwemo kuimarisha ushirikiano katika maeneo ya kilimo,
biashara na viwanda,” alisema rais huyo. Aidha, alisema uhusiano wa nchi
hizo mbili ni wa muda mrefu, kwani pamoja na umbali wa kijiografia
Tanzania ni nchi ya kwanza Afrika kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia na
Vietnam.
Alisema ziara hiyo ni moja ya njia za kudumisha na kuboresha zaidi
uhusiano na ushirikiano baina ya nchi hizo mbili. Rais huyo alisema
kwenye mazungumzo yake na Magufuli, wamekubaliana kushirikiana katika
maeneo yatakayonufaisha nchi zote. Maeneo hayo ni kilimo, biashara,
viwanda na mawasiliano. Pia walisaini mikataba ya kutowatoza kodi mara
mbili wawekezaji na wafanyabiashara wanaowekeza katika nchi hizo.
Aidha Rais huyo alisema katika kikao chake na Rais Magufuli pamoja na
mawaziri wa nchi zote mbili wamekubaliana kuanzisha tume ya pamoja
itakayosimamia masuala ya uhusiano na ushirikiano baina ya nchi hizo
mbili. Aidha marais hao walizungumzia masuala ya kimataifa ambapo wote
kwa pamoja walikubaliana suala la kuhakikisha amani na utulivu linapewa
kipaumbele na mataifa yote duniani.
“Tulikubaliana kuwa nchi zote zina wajibu wa kuhakikisha suala la
amani linapewa kipaumbele, ikiwemo na mataifa ya kimataifa kuwa mstari
wa mbele katika kuhamasisha na kutuliza vurugu zinazoibuka katika nchi
mbalimbali,” alisema. Alisisitiza kuwa amemwalika Rais Magufuli
kutembelea Vietnam wakati wowote. Tayari Marais wastaafu Benjamin Mkapa
na Jakaya Kikwete, walishafanya ziara katika nchi hiyo wakati wa utawala
wao.
Rais Sang aliyeongozana na ujumbe wa watu 51 ataendelea kuwepo nchini
kwa ajili ya kumalizia ziara yake katika maeneo mbalimbali, ikiwemo
kutembelea Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA).
WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewaalika wawekezaji kutoka
Vietnam na kuwahakikishia kuwa Tanzania ni nchi inayoheshimu uwekezaji
na kwamba Serikali imesaini mikataba mbalimbali ya kupinga kutaifisha
mali za wawekezaji.
Majaliwa aliyasema hayo Dar es Salaam jana kwenye kongomano baina ya
ujumbe wa Tanzania na Rais wa Vietnam, Truong Tan San aliyeongozana na
ujumbe wake katika ziara ya siku nne nchini na wafanyabiashara wa
Tanzania.
Waziri Majaliwa alisema Tanzania ni nchi yenye mazingira mazuri ya
uwekezaji katika nyanja mbalimbali na kusisitiza kwamba wanaotaka
kuwekeza nchini wanafurahia mazingira hayo na uwepo wa dhamana ya mitaji
waliyowekeza.
“Ukiwekeza Tanzania una uhakika wa usalama wa mtaji na uwekezaji wako
kwa sababu nchi imesaini mikataba mbalimbali ya kupinga utaifishaji
mali za wawekezaji na kuhimiza uwekezaji wa kigeni katika mazingira
salama na yenye amani,” alisema Majaliwa.
Alisema kila mara nchi imekuwa ikiboresha sheria na kuimarisha
ushirikishwaji wa sekta binafsi ili kuchochea mazingira ya uwekezaji kwa
lengo la kuimarisha uchumi na kuinua maisha ya wananchi wake.
Akizungumzia soko mara baada ya kuwekeza nchini, Waziri Majaliwa
alisema, wawekezaji wanaowekeza nchini wana uhakika wa masoko ya zaidi
ya watu milioni 300 waishio Mashariki na Kusini mwa Afrika, ambao
hufurahia kuwepo kwa nchi katika Jumuiya kama ya SADC na EAC.
Aidha, nchi zaidi ya sita ambazo hazina bahari hutegemea bandari ya
Tanzania kufanya biashara na masoko katika eneo hilo. Akizungumzia
uwekezaji kutoka nje ya nchi, Waziri Majaliwa alisema serikali imekua
ikiboresha mazingira ya uwekezaji na hiyo imeongeza uwekezaji kutoka
nje.
Alisema mfano mzuri ni uwekezaji wa Kampuni ya Viettel Tanzania Ltd, ambao ni wawekezaji kutoka Vietnam
Ndalichako: Vyeti Vya Form Six Vilivyo Katika Mfumo wa GPA Havitabadilishwa Kwenda Division
Serikali
imesema haina mpango wa kubadili vyeti vya wanafunzi waliomaliza kidato
cha sita mwaka jana kutoka kwenye mfumo wa alama za GPA kwenda
Divisheni.
Msimamo huo wa serikali, umetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako.
Amesema
serikali haina mpango wa kubadili mfumo huo wa vyeti kwani tangu awali
wanafunzi walisoma kwa mfumo wa GPA na vyeti vilitoka kwa mfumo huo.
“Hatuwezi
kubadili vyeti hivyo, isipokuwa vimehitajika kwa ajili ya marekebisho
madogo ambayo Katibu Mkuu wa Wizara, aliyasema lakini siyo kubadili
kwenda mfumo wa divisheni,” alisema.
Februari
mwaka huu, Baraza la Taifa la Mitihani (Necta), lilitangaza kusitishwa
kwa ugawaji wa vyeti vya kidato cha sita kwa wanafunzi waliohitimu mwaka
2015, huku likiagiza kuwa vile vilivyokwisha gawanywa kwa wahitimu hao
vinatakiwa kurejeshwa kwenye chombo hicho.
Hata
hivyo, Katibu Mtendaji wa Necta, Dk, Charles Msonde, hakubainisha
marekebisho ambayo wanatakiwa kuyafanya kwenye vyeti hivyo na badala
yake kudai baraza linataka kujiridhisha na baadhi ya vitu.
Hatua
hiyo ya kubadili vyeti hivyo iliibua utata mkubwa, huku baadhi ya wadau
wakiwamo maofisa elimu, wakihisi Necta huenda inalenga kuvibadili vyeti
hivyo kutoka kwenye mfumo wa wastani wa alama (GPA), kwenda kwenye ule
wa jumla (division).
Atupwa Jela Miaka 7 kwa Kumkata Mkewe Sehemu za Siri Ili Apate Mali
Kikoti blog
Mkazi
wa Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora, Mashaka Maziku (60) amehukumiwa
kifungo cha miaka saba jela kwa kosa la kumkata sehemu za siri mkewe
kwa imani za kishirikina ili apate mali.
Hakimu
Joctan Rushwela alisema jana kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa
Tabora imeridhishwa na ushahidi uliotolewa upande wa mashtaka.
Hakimu
Rushwela alisema anamhukumu mshtakiwa huyo kwenda jela ili iwe fundisho
kwa wengine wanaokuwa na tamaa ya kujipatia mali kwa njia za
kishirikina.
Awali
wakili wa Serikali, Idd Mgeni alidai kuwa mshtakiwa huyo na mganga wa
jadi, walitenda kosa hilo kati ya Oktoba 29 na Novemba 2, 2014 katika
eneo la Kazaroho Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora.
Wakati
wa tukio hilo, ilidaiwa kuwa Maziku aliambiwa na mganga huyo ambaye ni
mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo, Kahele Paul kwamba akipeleka sehemu
za siri za mkewe atapata Sh5milioni.
Alidai baada ya kupewa ushauri huo, alimchukua mkewe na kwenda kumnywesha pombe ili aweze kutimiza ukatili huo.
Alidai
baada ya kunywa pombe nyingi, alichukua kisu na kumkata sehemu za siri
mkewe na kuzihifadhi kwenye mfuko wa suruali yake na kutoweka.
Alidai
kwa mujibu wa mashahidi wanne, mwanamke huyo alikuwa akipiga kelele
kutokana na maumivu makali aliyopata huku akivuja damu nyingi.