ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 3 Februari 2017

MCH MSIGWA MBUNGE WA IRINGA ATOA MIL 1.5 KAMA MOTISHA TU KWA LIPULI FC.... we unasubiri nini?

Wakati kesho jumamosi timu ya wanaIringa Lipuli Fc inaingia katika mchezo wake muhimu wa kuingia kucheza ligi kuu ya VPL baada ya kuwa na uhakika wa kutwaa pointi 3 zilizosalia,  wadau  wa mbunge wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa ( Chadema) wameahidi kutoa motisha ya Tsh milioni 1.5 kwa timu ya Lipuli Fc .

Katika taarifa iliyotolewa na Mbunge Msigwa ambae yupo mjini Dodoma kuendelea na vikao vya bunge amesema yupo tayari kesho kuungana na wabunge wengine wa mkoa wa Iringa kuja kuishangilia timu ya Lipuli fc pamoja na mashabiki wengine.

Uzalendo huu ambao mbunge wetu aendelea kuonyesha ni wazi ligi kuu Iringa ipo mbioni kufanyika mkoani hapa  msimu ujao.

Tayari wabunge mbali mbali kama Ritta Kabati , Venance Mwamoto ,Costa Chumi, Mahamudu Mgimwa, Godfrey Mgimwa na wengine wameendelea kuisaidia timu ya Lipuli Fc .

Iwapo upo tayari kuchangia Lipuli Fc Tuma mchango wako kuanzia tshs 10,000/= kwenda namba 0713446699  na 0754695874  *zote Abousufian Silia..

Hakuna maoni: