ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumanne, 16 Juni 2015

Hii ndo elimu bora

Elimu Bora ni ile inayozingatia masuala yafuatayo;

Image result for elimu boraImage result for elimu bora 
Hali ya Wanafunzi
Je, wako tayari na wanaweza kushiriki katika elimu yao? Je, wanapata ushirikiano kutoka kwenye familia na jamii zao?
Mazingira ya Kujifunzia
Je, ni salama kwa watoto wote bila kujali jinsia, imani na ulemavu? Je, vifaa kama vile madawati, vyoo na vitabu vinatosheleza mahitaji yote?
Mambo yanayofundishwa Darasani
Ni aina ipi ya ujuzi ambao Mitaala inatilia mkazo? Je, maudhui yake yanaendana na mahitaji ya jamii? Je, yanakuza uelewano, umoja, amani na haki za binadamu?
Walimu na Ufundishaji
Je, kuna walimu wa kutosha na wako tayari kufundisha? Je, ufundishaji unamjali mwanafunzi, na mahuasiano kati ya wanafunzi na mwalimu darasani yakoje?
Matokeo ya Elimu
Wahitimu wana aina gani ya maarifa, ujuzi na mtazamo? Na wanayatumiaje katika maisha yao ndani ya jamii?

Jumatatu, 8 Juni 2015

Waliochukua fomu urais kupitia CCM wafikia 18


Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akionyesha begi lenye fomu za kuomba kugombea kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana. Picha na Edwin Mjwahuzi 
Na Sharon Sauwa, Mwananchi
Dodoma. Makada watatu wa CCM jana walijitokeza katika makao makuu yake mjini hapa kuchukua fomu kuomba kupewa ridhaa na chama hicho ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani
Waliochukua fomu jana ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, kada wa chama hicho, Leonce Mulenda na Ofisa Mwandamizi mstaafu wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), Peter Nyalali na kufanya idadi ya wanaCCM waliokwisha fanya hivyo kufikia 18.
Nyalandu: Ninafahamu changamoto
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Nyalandu ambaye alisindikizwa na wabunge wa viti maalumu, Mary Chatanda na Martha Mlata alisema amechukua fomu akifahamu umuhimu wa kuyaendeleza yote yaliyofanywa na serikali ya awamu ya nne... “Ninafahamu changamoto zinazotukabili. Nazitazama, naziona hatua ambazo zipo tangu wakati wa Baba wa Taifa alipomkabidhi kijiti Rais Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Rais Jakaya Kikwete.”
Alisema anafahamu changamoto zinazolikabili Taifa na anaitazama nchi iendelee kulinda misingi iliyoachwa na waasisi wa Taifa kwa kuendeleza amani.
Alisema umoja, undugu na mshikamano atakaoulinda, utaifanya Tanzania iwe na nguvu ya kutatua changamoto za sasa na za kesho.
Huku akipigiwa makofi na wapambe wake, Nyalandu alisema waliambiwa zamani kuwa wazee wanaotawala vyema wanastahili heshima maradufu.
“Tutaendelea kuwaenzi wazee waliotutawala, wamekuwa wakitulea katika miji na vijijini, tutaendelea kuwaangalia vijana na wanawake kwa kuangalia nini ambacho tumefanikiwa katika awamu hii ya Rais Kikwete. Tutaangalia mageuzi tutakayoyafanya ili kijana wa Kitanzania aonekane si mzigo,” alisema.
Alisema endapo atafanikiwa kupata nafasi hiyo, serikali yake itajikita katika kuinua uchumi wa nchi.
“Tutajikita katika kuwekeza katika rasilimali watu, kuwawezesha wananchi kiuchumi… na sisi wenyewe kama Taifa tutasimama kwa miguu yetu. Tutatembea vichwa vikiwa vimesimama imara tuishangaze dunia kwa pamoja,” alisema.
Jambo jingine ni kuimarisha vyombo vya ulinzi na usalama wa nchi kuhakikisha kuwa Taifa linakuwa na uwezo wa kujilinda na raia wake.
“Tutaendelea kuhakikisha mifumo ya matatizo ikiwa ni pamoja na magonjwa, tatizo la Ukimwi, mshtuko wa ebola tulioupata ambao ulitetemesha utalii duniani, changamoto za kigaidi, tutajipanga kama Taifa na kama umoja kuhakikisha tunakabiliana nazo,” alisema.

Nyalandu alisema njia bora ya kuwawezesha watu ni kuboresha mfumo wa elimu ambao umefanikiwa chini ya Serikali ya Awamu ya Nne.
Alisema  endapo atafanikiwa katika safari yake hiyo ya kuutafuta urais, atahakikisha kila shule ya msingi na sekondari inakuwa na kitengo cha mafunzo stadi.
Alipoulizwa iwapo chama kingine cha siasa kitashinda upande wa pili wa Muungano, alisema: “Ni muungano wa mapenzi ya ndani, ni muungano ambao unazidi tofauti zetu za dini, kabila na uwepo wa Bara na Visiwani na hali kadhalika, unazidi tofauti zetu za itikadi za vyama.”
Alisema atashirikiana na viongozi wa Zanzibar katika kuuenzi Muungano wa Tanzania ili uwe ishara ya amani na mshikamano.
Mulenda: Kipaumbele ni elimu bora
Mulenda (41) amechukua fomu ya kuwania kuteuliwa na chama chake kugombea urais huku akisema kipaumbele chake cha kwanza ni elimu bora.
Kada huyo ambaye alisindikizwa na watu wasiozidi sita, alisema kaulimbiu yake ni Serikali sikivu, makini na inayojali shida za watu.
Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo katika ofisi za Makao Makuu ya CCM, Mulenda alisema amejitathmini na kujipima kuwa anaweza kuwa kiongozi wa Tanzania. Alitaja vipaumbele vingine kuwa ni kuhakikisha CCM inakuwa imara zaidi.
“Kwa upande wa chama nitahakikisha  nasimamia kwa vitendo katiba ya chama, kanuni na taratibu bila kuacha sheria na miongozo inayoongoza nchi yetu,” alisema.
Alisema atasimamia uamuzi wa vikao na kuhakikisha unatekelezwa na kupima matokeo kwa kufanya tathmini juu ya malengo waliyojiwekea.
Mulenda alisema endapo atashinda na CCM ikawa ndicho chama tawala, atakuwa na kazi ya kuisimamia Serikali.
“Ukiona Serikali inafanya vibaya na chama kinachotawala kinaona sawasawa, basi siku za kukaa madarakani za chama hicho zinahesabika,” alisema.
Alisema endapo atafanikiwa katika safari yake hiyo, atahakikisha Serikali yake kupitia ilani ya uchaguzi ya CCM inakuwa sikivu, makini na inayojali shida za watu.
“Nawahakikishia wananchi kuwa kwa kutambua shida zao ni dhahiri nitajua wanataka nini na hawataki nini na kwa msingi huo, Serikali itakayokuwa chini yangu wakati wote tunahakikisha Watanzania tunawapeleka kule wanakotarajia kwa kutumia uwezo wetu ambao ulijengwa na waasisi wa Taifa hili,” alisema.
Alisema wazee waliwaambia kuwa nchi ina raslimali za kutosha na kinachotakiwa ni kujiongoza ili kutumia amani na utulivu kujenga nchi.

Ijumaa, 29 Mei 2015

Midahalo ya watangaza nia CCM sasa ruksa

07 June 2015

By Stella Nyemenohi, Bukoba

WATANZANIA sasa watapata fursa pana zaidi ya kufahamu kwa undani wanachama wa CCM waliotangaza nia ya kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama hicho, baada ya Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana, kuridhia midahalo kwa wanachama hao.
Akizungumza katika ziara ya siku 28 ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM na kuzungumza na Watanzania katika mikoa ya Kanda ya Ziwa jana, Kinana alisema hakuna kipingamizi kwa watangaza nia hao kwenda katika midahalo.
“Wanachama wetu wamealikwa kwenye midahalo, sasa wamenipigia simu na kuniuliza twende ama tusiende. Jibu langu hiari yao kwenda na ni hiari yao kutokwenda, kwa hiyo wana uhuru wa kwenda.
“Hawa walipotangaza nia walisema mengi sana, ni sawa sawa na mdahalo mwingine, walipochukua fomu walikutana na waandishi wa habari walisema mengi sana, huo nao ni mdahalo mwingine, huko wanakopita kupata wadhamini, wanasema mengi nayo ni midahalo, kwa nini sisi tukatae mdahalo ambao watu wameomba?
“Walialikwa kwa barua, wakanipigia wakasema wameshakubali waende wasiende, nimewaambia ruksa nenda wakitaka, lakini CCM haiandai mdahalo, CCM haimtumi mtu na CCM haimnyimi mtu, hiari ni yao,” alisema Kinana.
Uamuzi huo wa Kinana umekuja siku moja baada ya kutolewa kwa taarifa ya katazo kwa watangaza nia hao kushiriki katika midahalo hiyo.
Katazo hilo lilitolewa juzi na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM ya Oganaizesheni, Dk Muhammed Seif Khatib, ambaye alisema chama hicho hakiruhusu midahalo kwa makada wake hao, kwa kuwa hakina mgombea mpaka sasa.
Nafasi ya Watanzania Akifafanua zaidi kuhusu umuhimu wa midahalo kwa watangaza nia hao, Kinana ambaye ameshazungumza mara nyingi kuwa nafasi ya urais ni kubwa, hivyo kunahitajika umakini kumpata mrithi wa Rais Jakaya Kikwete, alisema ni vizuri wanaCCM na Watanzania watumie midahalo hiyo kupima watangaza nia hao.
“Hawa wanaoomba nafasi kupitia CCM, nafasi wanayoomba ni kuongoza Watanzania, kwa hiyo kama kuna mdahalo utakaosaidia watu kujibu maswali, kueleza sera zao na kutoa ufafanuzi kwa masuala mbalimbali, wanachama wa CCM wakapima vizuri zaidi na wananchi wakatumia nafasi hiyo kupima na kuwaelewa vizuri zaidi, hakuna ubaya.
“Lengo la mdahalo iwe kwa Watanzania kufahamu wagombea vizuri zaidi, kufahamu sera zao, kuwapima vizuri zaidi uwezo wao wa kujenga hoja,” alisisitiza.
Hadhari Hata hivyo, Kinana hakuacha kutoa hadhari kwa waandaaji wa midahalo na kuwaomba waandae midahalo hiyo kwa kuzingatia haki ili lengo liwe kutoa fursa kwa wana CCM na Watanzania, ya kuwafahamu na kuwaelewa zaidi wagombea hao na kamwe isiwe sababu ya kujenga mifarakano isiyo na sababu.
Maandalizi Kwa hatua hiyo ya Kinana, sasa Taasisi ya CEO Round Table Tanzania (CEOrt), iliyoandaa midahalo hiyo, itaendelea na ratiba yake kesho kwa watangaza nia sita wa kwanza waliothibitisha kushiriki.
Kwa mujibu wa taarifa za CEOrt zilizotolewa mwishoni mwa wiki, watangaza nia waliothibitisha kushiriki ni sita na mdahalo huo utafanyika mara tatu, mara ya pili ukihusisha watangaza nia wa vyama vya upinzani hasa kutoka muungano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), unaoundwa na vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD na mara ya tatu utahusu watangaza nia wengine kutoka CCM.
Watangaza nia watakaoanza kesho katika mdahalo utakaorushwa moja kwa moja na luninga mbalimbali za hapa nchini, utawahusisha aliyekuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye na mmoja wa wanadiplomasia wakubwa nchini ambaye pia ndiye mwanamke pekee, Balozi Amina Salum Ali.
Wengine ni Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Tekinolojia, January Makamba; Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta; Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba.
Hoja kiongozi Akizungumza kuhusu mdahalo huo katika redio ya Clouds FM mwishoni mwa wiki, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa CEOrt, Ali Mufuruki alisema mdahalo huo utakuwa na muongoza mdahalo (moderator) na kutakuwa na maswali ambayo watangaza nia hao watayajibu.
Mbali na maswali hayo yatakayotokana na hoja mbili mahususi; mosi kipaumbele chao cha uchumi katika kipindi cha mwaka 2015 mpaka 2020 na pili mikakati yao katika jitihada za kuhakikisha kunakuwepo utawala bora na kushinda vita dhidi ya rushwa, moderator huyo atakuwa na fursa ya kuuliza maswali zaidi, ili kupata ufafanuzi wa kina kutoka kwao.
Licha ya hoja hizo mbili mahususi, pia watangaza nia hao wanatarajiwa kuzungumza kuhusu malengo yao ya muda mrefu yatakayoleta maendeleo na kutunza utajiri wa maliasili ya Tanzania.
Pia walitarajiwa watoe maoni yao kuhusu dira zao, mikakati na jitihada za kuipeleka Tanzania katika mambo muhimu yatakayoharakisha uchumi wa muda mrefu.
Washiriki wa mdahalo huo kwa mujibu wa Mufuruki, ni watu mbalimbali kutoka sekta binafsi na katika umma wa Watanzania kwa ujumla, lakini watatakiwa kulipia kiingilio cha Sh 100,000.
Kwa mujibu wa Mufuruki, mpaka mwishoni mwa wiki kulikuwa na kasi nzuri ya washiriki waliokuwa wamekwishalipia kiingilio na wengine wakiwasiliana na waandaaji kwa ajili ya kulipa kiingilio, ambapo alihadharisha kuwa nafasi ni chache kwa kuwa ukumbi wa mjadala unachukua watu wasiozidi 300.
Waliochukua fomu Mpaka jana wana CCM 14 walikuwa wamechukua fomu, baada ya watatu kuchukua juzi na mmoja jana, ambaye ni Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba. Mwanachama Mussa Godwin Mwapango naye alitarajiwa kuchukua fomu jana.
Waliochukua juzi ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani. Wanachama wengine 10 walichukua kuanzia Jumatano iliyopita ambayo ilikuwa siku ya kwanza ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira.
Wengine ni Balozi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika (AU) katika Marekani, Amina Salum Ali na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere ambaye ni mtoto wa Mwalimu Nyerere.
Pia mawaziri wakuu wa zamani Frederick Sumaye na Edward Lowassa, Makamu wa Rais Dk Mohammed Gharib Bilal, Balozi mstaafu Ali Abeid Karume - mtoto wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Abeid Amaan Karume na Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli, Mussa Godwin Mwapango.
Waliokwisha kutangaza nia ambao hawajachukua fomu ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia January Makamba, wabunge William Ngeleja (Sengerema), Dk Hamis Kigwangalla (Nzega) na Luhaga Mpina (Kisesa).
(source habari leo)

 




Jumatatu, 25 Mei 2015

Nini tatizo la Migomo vyuo vikuu-

 Na mwandishi wetu  kazinde

 


Mara kadhaa matatizo haya ya wanafunzi kucheleweshewa fedha zao yamekuwa yakiibuka na imekuwa ni kawaida kwa Serikali kutumia vyombo vyake vya dola kuwatuliza, huku baadhi wakikamatwa na kufunguliwa kesi au kuachiwa kwa tuhuma za kukiuka sheria wakati wa kudai haki zao.
Hata hivyo, matatizo yanapoisha na jitihada za kutafuta suluhisho la kudumu la matatizo yao huishia hapo hapo hadi tatizo jingine linapozuka. Kibaya zaidi ni pale Jeshi la Polisi linalolazimishwa kutumia nguvu za ziada katika kudhibiti wanafunzi na kusababisha baadhi kujeruhiwa, kupotezewa muda zaidi wa masomo na hata kujenga chuki dhidi ya Serikali yao.

Mwanachuo mmoja wa chuo kikuu MKWAWA alikuwa na majibu haya alipokuwa akihojiwa na kituo cha redio EBON FM Iringa
mi nafikiri wanafunzi wengi wanagoma kwasababu madai yao yanashindwa kutatuliwa kwa wakati sitahili mfano wanafunzi wanapodai fedha za kujikimu lakini sababu zinazotolewa zinakuwa hazina msingi ndani yake  na hii mara nyingi inatokana na baadhi ya viongozi waliokabidhiwa dhamana katika idara husika kushindwa kufuatilia fedha kwa wakati na wengine kushindwa kuwajibika

NINI SULUHU YA TATIZO HILO
Kombe Godwin anasema, hatuna budi kubadili mfumo mzima wa watu wasio wajibika ambao wanafanya kazi kwa mazoea na njia pekee ni kuimarisha mifumo ya kiutendaji  kwa kuondoa mfomo uliopo sasa na suala la kutumia nguvu Kuzuia maandamano hakutatui matatizo ya wanafunzi na kutumia nguvu za ziada kudhibiti wanafunzi wanaogoma hakutatui matatizo yao. Kinachotakiwa ni Serikali kujipanga kuhakikisha matatizo hayo hayaibuki na kusababisha wanafunzi watumie haki yao ya kugoma au kuandamana.

JE JITIHADA ZINACHUKULIWA
Inashangaza kuona kwamba hadi leo aliyechelewesha fedha hizo ameachwa bila ya hata kutingishwa wakati waliogoma hadi kufanya fujo kutokana na kucheleweshwa kwa fedha hizo wamesimamishwa masomo, kupigwa na hata kufunguliwa mashtaka. Kwa utamaduni huu nchi itakwenda kweli

JE WANACHUO NAO WAFANYEJE KUDAI HAKI
Pamoja na hayo, wanafunzi pia wanatakiwa waanike matatizo yao kwa njia ambayo haitaharibu miundombinu ambayo wanaitumia kwenye masomo na ambayo itatumiwa na vizazi kadhaa vijavyo. Kufanya fujo na uharibifu ni kutowajibika pia kwa nchi yao na vizazi vinavyowafuata

Ijumaa, 22 Mei 2015

LOWASA HURU KUENDELEA NA KAZI ZA KISIASA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kamati Kuu imepokea na kutafakari taarifa ya Kamati ya Usalama na Maadili ambayo ilipitia adhabu waliyopewa wanachama sita waliokiuka kanuni za Maadili na kupewa Onyo Kali, adhabu iliyodumu kwa kipindi kisichopungua miezi 12.
Wanachama hao sita ni;-
i. January Makamba
ii. Willium Ngeleja
iii. Steven Wasira
iv. Bernard Membe
v. Edward Lowassa
vi. Fredrick Sumaye
Kamati Kuu imepokea na kukubali pendekezo la Kamati ya Usalama na Maadili ya kumalizaka kwa kipindi cha adhabu kwa wanachama hawa. Kwahiyo adhabu hiyo kwa sasa imemalizika, na wanachama hao wameruhusiwa kuendelea na shughuli zao katika Chama.
Hata hivyo Kamati Kuu inawataka wanachama hawa na wale wengine wenye nia ya kugombea Urais kupitia CCM Kuzisoma , Kuziheshimu na Kuzizingatia Kanuni za Maadili za CCM na kanuni zingine zinazoongoza mchakato ndani ya Chama, ili wasikumbwe na adhabu itokanayo na kuzivunja kanuni hizo.
Wale wote wanaotaka kugombea, yaani waliokuwa kwenye adhabu na wengine watakaojiingiza kwenye kampeni mapema na hivyo kukiuka maadili na miiko ya Chama, taarifa za kukiuka kwao zitatumiwa wakati wa kuchuja majina ya wagombea utakapofika.
Taarifa hizo zitatumika katika kuwapima na kuamua iwapo wana sifa za kutosha na wanafaa au hawafai katika kupata uteuzi wa nafasi wanayoiomba.
Imetolewa na;-
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi
22/05/2015

MGOMO wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)

 Na waandishi wetu(Longo na Msuya) kutoka Dodoma;
wanafunzi wa  chou kikuu cha DODOMA wamegoma sababu Kushereweshwa kwa  fedha za kujikimu.. wanafunzi wengi wanatoka maeneo ya vijijini watoto wa maskini,  wanafunzi hao wamegoma na kufanya maandamano ambayo yaliwaza kuzua mapambano baina ya askari FFU na wananachuo hiyo imekuja siku moja baada ya naibu waziri kutoa majibu haya

Niwaombe radhi wanafunzi wa vyuo vikuu.. Tuliongea na viongozi wa vyuo pamoja na bodi na Wizara inayosimamia, kulikuwepo na utaratibu wa kuipa fedha hizo na mpaka jana tayari fedha ilishatoka Wizara ya fedha.. wataalamu ambao wanashughulikia kuzifikisha hizo fedha kwa wanafunzi watoe kwanzaq fedha hizo ndio wakae vikao kuliko kusubiri kupitisha kwa utaratibu ambao wanafunzi wataendelea kupata shida”

“Serikali tunajitahidi kuhakikisha kwamba tunawafikishia kwa wakati fedha.. Serikali imeshatoa fedha na taasisi zinakopita wajitahidi leo leo vyuo vyote viwe vimeshapata fedha hizo”
 hivi ndivo hali ilivokuwa chuo kikuu DODOMA leo
  
FFU WAKIANDAA ULINZI 
 
Wanachuo wakiwa tayari kwa maandamano
 
wanachuo wakisubiri utaratibu
 
wanachuo wakiwa kwenye makundi
 
Mapamano yakianza kati ya polisi na wanachuo

Hatima ya makada sita wa CCM leo

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Jakaya Mrisho Kikwete 
Kwa ufupi
Kwa mara ya kwanza, CCM inakabiliwa na kazi ngumu ya kuamua hatima ya makada iliowafungiwa katika kipindi muhimu cha kuteua mgombea mpya wa urais kutokana na mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Jakaya Kikwete kutoweza kugombea nafasi hiyo kwa kipindi cha tatu kutokana na matakwa ya kikatiba.
 
Dodoma. Kamati Kuu ya CCM, ambayo ndiyo inaanzisha mambo yote muhimu ya chama hicho, leo inakutana kuandaa ajenda za mkutano wa Halmashauri Kuu, huku suala linalosubiriwa kwa hamu likiwa ni hatima ya makada sita wanaotajwa kuwania urais ambao wanatumikia adhabu ya kuzuiwa kujihusisha na uchaguzi.
Kwa mara ya kwanza, CCM inakabiliwa na kazi ngumu ya kuamua hatima ya makada iliowafungiwa katika kipindi muhimu cha kuteua mgombea mpya wa urais kutokana na mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Jakaya Kikwete kutoweza kugombea nafasi hiyo kwa kipindi cha tatu kutokana na matakwa ya kikatiba.
Mmoja wa watu walio karibu na uongozi wa chama hicho aliiambia Mwananchi jana kuwa CCM imejikita zaidi katika kutafuta mwanachama atakayekipa ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu, lakini suala la makada waliofungiwa ambao baadhi yao wanapewa nafasi kubwa ya kupitishwa, halitachukua muda mrefu kulijadili.
Kikao hicho kitafanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu uliopo jengo la makao makuu ya CCM mjini hapa, maarufu kama White House mjini Dodoma.
Ukumbi huo una historia ya muda mrefu ndani ya CCM ya kutolewa kwa uamuzi mgumu katika matukio kadhaa ya kisiasa, ukiwamo ule ulioweka historia ya Aboud Jumbe kuingia akiwa Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, lakini akatoka bila cheo chochote mwaka 1984.
Pia kwenye ukumbi huo kulifanyika uamuzi wa mambo mengine makubwa, hasa nyakati za kuchuja wagombea urais au uongozi wa chama, mambo ambayo pia yanaweza kutokea katika vikao vinavyoanza leo au vya baadaye.
Alipoulizwa kuhusu kikao hicho jana, katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema Rais Kikwete ataongoza kikao cha leo kilichopangwa kuanzia saa 4:00 asubuhi na kwamba maandalizi yamekamilika, huku baadhi ya wajumbe wakiwa wameshawasili.
Alipoulizwa kuhusu nini wategemee wanachama na wananchi, Nape alijibu kwa kifupi kuwa watarajie kuwa “CCM watatoka wakiwa kitu kimoja” kuliko inavyotarajiwa na wengi.
Hata hivyo, mbali na hofu kuhusu hatua za kinidhamu kwa wajumbe walioadhibiwa kwa kuanza kampeni mapema na kukiuka maadili, taarifa nyingine kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa vikao hivyo zilidai kuwa mkutano huo utajikita zaidi kuangalia utaratibu mzima wa kuchukua fomu za wagombea wote wa urais, ubunge na udiwani.
“Vikao hivi vinaangalia utaratibu tu wa jinsi ya kuchukua fomu na wala havitagusia suala la mchujo wa wagombea urais wala ubunge,” alisema mtoa taarifa huyo.
Kamati Kuu imetanguliwa na vikao vya mfululizo vya Sekretarieti na Kamati ndogo ya Kanuni.
Kamati ya Kanuni na Maadili ilitarajiwa kukutana jana usiku au leo asubuhi kabla ya Kamati Kuu
Mtoa taarifa mwingine ambaye ni mjumbe wa NEC, alidokeza kuwa vikao hivyo havitajikita sana na uchujaji wa majina ya wagombea urais, badala yake kwa kuwa muda umekwenda, wameamua kushughulikia ratiba kwa ajili ya uchukuaji wa fomu za wagombea wa ngazi zote za uchaguzi ili nao wapate muda wa kwenda kutafuta wadhamini kabla ya mchujo.
Hata hivyo, mtoa habari mwingine kutoka ndani ya CCM, alisema licha ya kushughulikia masuala ya ratiba, kanuni na kuangalia ilani, bado suala la mchujo wa wagombea ni tata na huenda wakaangalia mgombea ambaye anaweza kukipa ushindi chama kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa huyo, hoja ya watangaza nia sita ya kukiuka kanuni za chama haitakipotezea muda, zaidi ya kuangalia nani anaweza kukipa chama ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Taarifa za ndani kutoka kwa mmoja wa wajumbe wa vikao hivyo vya juu vya CCM alidokeza kuwa kwa hali ya sasa ya kisiasa na joto linavyozidi kupanda hasa kasi ya Ukawa, CCM itafanya kama ilivyofanya kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 wakati Kamati ya Usalama na Maadili ilipokwenda Zanzibar ikiwa na faili la tuhuma za mmoja wa wagombea, lakini vikao vilijikita kwenye mgombea ambaye angekipa ushindi chama.
Kwa mujibu wa taarifa hizo mambo mengi hasa malalamiko ya ukiukwaji wa maadili wa baadhi ya viongozi ngazi za chini, yatamalizwa na Kamati Kuu na yale yatakayohitaji uamuzi wa mamlaka za uteuzi yatapelekwa Halmashauri Kuu.
Mtoa taarifa huyo alisema suala la Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Paul Makonda na makada wawili CCM, Mgana Msindai ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho mkoani Singida, na John Guninita, ambao wamefungua kesi ya madai mahakamani, linaweza kuibua mjadala.
Hivi karibuni Nape alikaririwa akisema kuwa chama hicho katika kushughulikia matatizo yote yaliyojitokeza kitatumia kanuni zake na hakuna atakayeonewa.
“Nasisitiza ni kanuni na wala si mimi, nasisitiza pia kuwa sijazuia watu kuchukua fomu bali chama kinafuata kanuni,” alisema.
Alisema kada yeyote wa CCM akiamua kufanya kampeni kabla ya muda ataadhibiwa, lakini akisubiri hana hatia kwani kinachongomba ni kanuni.
Maelezo hayo ya Nape yalikuwa yanalenga uamuzi wa Kamati Kuu ya CCM kuwafungia kwa miezi 12 vigogo wa chama hicho uliotolewa Februari mwaka jana kwa kuanza kampeni kabla ya wakati na kikiuka maadili ya chama.
Wakati huo huo, hoteli na nyumba za kulala wageni zimejaa na hiyo kufanya baadhi ya wageni wanaoingia mkoani hapa kulazimika kutafuta malazi nje ya mji.
Uchunguzi wa gazeti hili uliofanywa wa nyumba za kulala wageni katikati ya mji umebaini kuwa wageni waliojaza nyumba hizo ni wajumbe na wapambe.(Source Mwananchi)