ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 29 Mei 2015

Midahalo ya watangaza nia CCM sasa ruksa

07 June 2015

By Stella Nyemenohi, Bukoba

WATANZANIA sasa watapata fursa pana zaidi ya kufahamu kwa undani wanachama wa CCM waliotangaza nia ya kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama hicho, baada ya Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana, kuridhia midahalo kwa wanachama hao.
Akizungumza katika ziara ya siku 28 ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM na kuzungumza na Watanzania katika mikoa ya Kanda ya Ziwa jana, Kinana alisema hakuna kipingamizi kwa watangaza nia hao kwenda katika midahalo.
“Wanachama wetu wamealikwa kwenye midahalo, sasa wamenipigia simu na kuniuliza twende ama tusiende. Jibu langu hiari yao kwenda na ni hiari yao kutokwenda, kwa hiyo wana uhuru wa kwenda.
“Hawa walipotangaza nia walisema mengi sana, ni sawa sawa na mdahalo mwingine, walipochukua fomu walikutana na waandishi wa habari walisema mengi sana, huo nao ni mdahalo mwingine, huko wanakopita kupata wadhamini, wanasema mengi nayo ni midahalo, kwa nini sisi tukatae mdahalo ambao watu wameomba?
“Walialikwa kwa barua, wakanipigia wakasema wameshakubali waende wasiende, nimewaambia ruksa nenda wakitaka, lakini CCM haiandai mdahalo, CCM haimtumi mtu na CCM haimnyimi mtu, hiari ni yao,” alisema Kinana.
Uamuzi huo wa Kinana umekuja siku moja baada ya kutolewa kwa taarifa ya katazo kwa watangaza nia hao kushiriki katika midahalo hiyo.
Katazo hilo lilitolewa juzi na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM ya Oganaizesheni, Dk Muhammed Seif Khatib, ambaye alisema chama hicho hakiruhusu midahalo kwa makada wake hao, kwa kuwa hakina mgombea mpaka sasa.
Nafasi ya Watanzania Akifafanua zaidi kuhusu umuhimu wa midahalo kwa watangaza nia hao, Kinana ambaye ameshazungumza mara nyingi kuwa nafasi ya urais ni kubwa, hivyo kunahitajika umakini kumpata mrithi wa Rais Jakaya Kikwete, alisema ni vizuri wanaCCM na Watanzania watumie midahalo hiyo kupima watangaza nia hao.
“Hawa wanaoomba nafasi kupitia CCM, nafasi wanayoomba ni kuongoza Watanzania, kwa hiyo kama kuna mdahalo utakaosaidia watu kujibu maswali, kueleza sera zao na kutoa ufafanuzi kwa masuala mbalimbali, wanachama wa CCM wakapima vizuri zaidi na wananchi wakatumia nafasi hiyo kupima na kuwaelewa vizuri zaidi, hakuna ubaya.
“Lengo la mdahalo iwe kwa Watanzania kufahamu wagombea vizuri zaidi, kufahamu sera zao, kuwapima vizuri zaidi uwezo wao wa kujenga hoja,” alisisitiza.
Hadhari Hata hivyo, Kinana hakuacha kutoa hadhari kwa waandaaji wa midahalo na kuwaomba waandae midahalo hiyo kwa kuzingatia haki ili lengo liwe kutoa fursa kwa wana CCM na Watanzania, ya kuwafahamu na kuwaelewa zaidi wagombea hao na kamwe isiwe sababu ya kujenga mifarakano isiyo na sababu.
Maandalizi Kwa hatua hiyo ya Kinana, sasa Taasisi ya CEO Round Table Tanzania (CEOrt), iliyoandaa midahalo hiyo, itaendelea na ratiba yake kesho kwa watangaza nia sita wa kwanza waliothibitisha kushiriki.
Kwa mujibu wa taarifa za CEOrt zilizotolewa mwishoni mwa wiki, watangaza nia waliothibitisha kushiriki ni sita na mdahalo huo utafanyika mara tatu, mara ya pili ukihusisha watangaza nia wa vyama vya upinzani hasa kutoka muungano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), unaoundwa na vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD na mara ya tatu utahusu watangaza nia wengine kutoka CCM.
Watangaza nia watakaoanza kesho katika mdahalo utakaorushwa moja kwa moja na luninga mbalimbali za hapa nchini, utawahusisha aliyekuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye na mmoja wa wanadiplomasia wakubwa nchini ambaye pia ndiye mwanamke pekee, Balozi Amina Salum Ali.
Wengine ni Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Tekinolojia, January Makamba; Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta; Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba.
Hoja kiongozi Akizungumza kuhusu mdahalo huo katika redio ya Clouds FM mwishoni mwa wiki, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa CEOrt, Ali Mufuruki alisema mdahalo huo utakuwa na muongoza mdahalo (moderator) na kutakuwa na maswali ambayo watangaza nia hao watayajibu.
Mbali na maswali hayo yatakayotokana na hoja mbili mahususi; mosi kipaumbele chao cha uchumi katika kipindi cha mwaka 2015 mpaka 2020 na pili mikakati yao katika jitihada za kuhakikisha kunakuwepo utawala bora na kushinda vita dhidi ya rushwa, moderator huyo atakuwa na fursa ya kuuliza maswali zaidi, ili kupata ufafanuzi wa kina kutoka kwao.
Licha ya hoja hizo mbili mahususi, pia watangaza nia hao wanatarajiwa kuzungumza kuhusu malengo yao ya muda mrefu yatakayoleta maendeleo na kutunza utajiri wa maliasili ya Tanzania.
Pia walitarajiwa watoe maoni yao kuhusu dira zao, mikakati na jitihada za kuipeleka Tanzania katika mambo muhimu yatakayoharakisha uchumi wa muda mrefu.
Washiriki wa mdahalo huo kwa mujibu wa Mufuruki, ni watu mbalimbali kutoka sekta binafsi na katika umma wa Watanzania kwa ujumla, lakini watatakiwa kulipia kiingilio cha Sh 100,000.
Kwa mujibu wa Mufuruki, mpaka mwishoni mwa wiki kulikuwa na kasi nzuri ya washiriki waliokuwa wamekwishalipia kiingilio na wengine wakiwasiliana na waandaaji kwa ajili ya kulipa kiingilio, ambapo alihadharisha kuwa nafasi ni chache kwa kuwa ukumbi wa mjadala unachukua watu wasiozidi 300.
Waliochukua fomu Mpaka jana wana CCM 14 walikuwa wamechukua fomu, baada ya watatu kuchukua juzi na mmoja jana, ambaye ni Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba. Mwanachama Mussa Godwin Mwapango naye alitarajiwa kuchukua fomu jana.
Waliochukua juzi ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani. Wanachama wengine 10 walichukua kuanzia Jumatano iliyopita ambayo ilikuwa siku ya kwanza ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira.
Wengine ni Balozi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika (AU) katika Marekani, Amina Salum Ali na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere ambaye ni mtoto wa Mwalimu Nyerere.
Pia mawaziri wakuu wa zamani Frederick Sumaye na Edward Lowassa, Makamu wa Rais Dk Mohammed Gharib Bilal, Balozi mstaafu Ali Abeid Karume - mtoto wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Abeid Amaan Karume na Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli, Mussa Godwin Mwapango.
Waliokwisha kutangaza nia ambao hawajachukua fomu ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia January Makamba, wabunge William Ngeleja (Sengerema), Dk Hamis Kigwangalla (Nzega) na Luhaga Mpina (Kisesa).
(source habari leo)

 




Jumatatu, 25 Mei 2015

Nini tatizo la Migomo vyuo vikuu-

 Na mwandishi wetu  kazinde

 


Mara kadhaa matatizo haya ya wanafunzi kucheleweshewa fedha zao yamekuwa yakiibuka na imekuwa ni kawaida kwa Serikali kutumia vyombo vyake vya dola kuwatuliza, huku baadhi wakikamatwa na kufunguliwa kesi au kuachiwa kwa tuhuma za kukiuka sheria wakati wa kudai haki zao.
Hata hivyo, matatizo yanapoisha na jitihada za kutafuta suluhisho la kudumu la matatizo yao huishia hapo hapo hadi tatizo jingine linapozuka. Kibaya zaidi ni pale Jeshi la Polisi linalolazimishwa kutumia nguvu za ziada katika kudhibiti wanafunzi na kusababisha baadhi kujeruhiwa, kupotezewa muda zaidi wa masomo na hata kujenga chuki dhidi ya Serikali yao.

Mwanachuo mmoja wa chuo kikuu MKWAWA alikuwa na majibu haya alipokuwa akihojiwa na kituo cha redio EBON FM Iringa
mi nafikiri wanafunzi wengi wanagoma kwasababu madai yao yanashindwa kutatuliwa kwa wakati sitahili mfano wanafunzi wanapodai fedha za kujikimu lakini sababu zinazotolewa zinakuwa hazina msingi ndani yake  na hii mara nyingi inatokana na baadhi ya viongozi waliokabidhiwa dhamana katika idara husika kushindwa kufuatilia fedha kwa wakati na wengine kushindwa kuwajibika

NINI SULUHU YA TATIZO HILO
Kombe Godwin anasema, hatuna budi kubadili mfumo mzima wa watu wasio wajibika ambao wanafanya kazi kwa mazoea na njia pekee ni kuimarisha mifumo ya kiutendaji  kwa kuondoa mfomo uliopo sasa na suala la kutumia nguvu Kuzuia maandamano hakutatui matatizo ya wanafunzi na kutumia nguvu za ziada kudhibiti wanafunzi wanaogoma hakutatui matatizo yao. Kinachotakiwa ni Serikali kujipanga kuhakikisha matatizo hayo hayaibuki na kusababisha wanafunzi watumie haki yao ya kugoma au kuandamana.

JE JITIHADA ZINACHUKULIWA
Inashangaza kuona kwamba hadi leo aliyechelewesha fedha hizo ameachwa bila ya hata kutingishwa wakati waliogoma hadi kufanya fujo kutokana na kucheleweshwa kwa fedha hizo wamesimamishwa masomo, kupigwa na hata kufunguliwa mashtaka. Kwa utamaduni huu nchi itakwenda kweli

JE WANACHUO NAO WAFANYEJE KUDAI HAKI
Pamoja na hayo, wanafunzi pia wanatakiwa waanike matatizo yao kwa njia ambayo haitaharibu miundombinu ambayo wanaitumia kwenye masomo na ambayo itatumiwa na vizazi kadhaa vijavyo. Kufanya fujo na uharibifu ni kutowajibika pia kwa nchi yao na vizazi vinavyowafuata

Ijumaa, 22 Mei 2015

LOWASA HURU KUENDELEA NA KAZI ZA KISIASA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kamati Kuu imepokea na kutafakari taarifa ya Kamati ya Usalama na Maadili ambayo ilipitia adhabu waliyopewa wanachama sita waliokiuka kanuni za Maadili na kupewa Onyo Kali, adhabu iliyodumu kwa kipindi kisichopungua miezi 12.
Wanachama hao sita ni;-
i. January Makamba
ii. Willium Ngeleja
iii. Steven Wasira
iv. Bernard Membe
v. Edward Lowassa
vi. Fredrick Sumaye
Kamati Kuu imepokea na kukubali pendekezo la Kamati ya Usalama na Maadili ya kumalizaka kwa kipindi cha adhabu kwa wanachama hawa. Kwahiyo adhabu hiyo kwa sasa imemalizika, na wanachama hao wameruhusiwa kuendelea na shughuli zao katika Chama.
Hata hivyo Kamati Kuu inawataka wanachama hawa na wale wengine wenye nia ya kugombea Urais kupitia CCM Kuzisoma , Kuziheshimu na Kuzizingatia Kanuni za Maadili za CCM na kanuni zingine zinazoongoza mchakato ndani ya Chama, ili wasikumbwe na adhabu itokanayo na kuzivunja kanuni hizo.
Wale wote wanaotaka kugombea, yaani waliokuwa kwenye adhabu na wengine watakaojiingiza kwenye kampeni mapema na hivyo kukiuka maadili na miiko ya Chama, taarifa za kukiuka kwao zitatumiwa wakati wa kuchuja majina ya wagombea utakapofika.
Taarifa hizo zitatumika katika kuwapima na kuamua iwapo wana sifa za kutosha na wanafaa au hawafai katika kupata uteuzi wa nafasi wanayoiomba.
Imetolewa na;-
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi
22/05/2015

MGOMO wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)

 Na waandishi wetu(Longo na Msuya) kutoka Dodoma;
wanafunzi wa  chou kikuu cha DODOMA wamegoma sababu Kushereweshwa kwa  fedha za kujikimu.. wanafunzi wengi wanatoka maeneo ya vijijini watoto wa maskini,  wanafunzi hao wamegoma na kufanya maandamano ambayo yaliwaza kuzua mapambano baina ya askari FFU na wananachuo hiyo imekuja siku moja baada ya naibu waziri kutoa majibu haya

Niwaombe radhi wanafunzi wa vyuo vikuu.. Tuliongea na viongozi wa vyuo pamoja na bodi na Wizara inayosimamia, kulikuwepo na utaratibu wa kuipa fedha hizo na mpaka jana tayari fedha ilishatoka Wizara ya fedha.. wataalamu ambao wanashughulikia kuzifikisha hizo fedha kwa wanafunzi watoe kwanzaq fedha hizo ndio wakae vikao kuliko kusubiri kupitisha kwa utaratibu ambao wanafunzi wataendelea kupata shida”

“Serikali tunajitahidi kuhakikisha kwamba tunawafikishia kwa wakati fedha.. Serikali imeshatoa fedha na taasisi zinakopita wajitahidi leo leo vyuo vyote viwe vimeshapata fedha hizo”
 hivi ndivo hali ilivokuwa chuo kikuu DODOMA leo
  
FFU WAKIANDAA ULINZI 
 
Wanachuo wakiwa tayari kwa maandamano
 
wanachuo wakisubiri utaratibu
 
wanachuo wakiwa kwenye makundi
 
Mapamano yakianza kati ya polisi na wanachuo

Hatima ya makada sita wa CCM leo

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Jakaya Mrisho Kikwete 
Kwa ufupi
Kwa mara ya kwanza, CCM inakabiliwa na kazi ngumu ya kuamua hatima ya makada iliowafungiwa katika kipindi muhimu cha kuteua mgombea mpya wa urais kutokana na mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Jakaya Kikwete kutoweza kugombea nafasi hiyo kwa kipindi cha tatu kutokana na matakwa ya kikatiba.
 
Dodoma. Kamati Kuu ya CCM, ambayo ndiyo inaanzisha mambo yote muhimu ya chama hicho, leo inakutana kuandaa ajenda za mkutano wa Halmashauri Kuu, huku suala linalosubiriwa kwa hamu likiwa ni hatima ya makada sita wanaotajwa kuwania urais ambao wanatumikia adhabu ya kuzuiwa kujihusisha na uchaguzi.
Kwa mara ya kwanza, CCM inakabiliwa na kazi ngumu ya kuamua hatima ya makada iliowafungiwa katika kipindi muhimu cha kuteua mgombea mpya wa urais kutokana na mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Jakaya Kikwete kutoweza kugombea nafasi hiyo kwa kipindi cha tatu kutokana na matakwa ya kikatiba.
Mmoja wa watu walio karibu na uongozi wa chama hicho aliiambia Mwananchi jana kuwa CCM imejikita zaidi katika kutafuta mwanachama atakayekipa ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu, lakini suala la makada waliofungiwa ambao baadhi yao wanapewa nafasi kubwa ya kupitishwa, halitachukua muda mrefu kulijadili.
Kikao hicho kitafanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu uliopo jengo la makao makuu ya CCM mjini hapa, maarufu kama White House mjini Dodoma.
Ukumbi huo una historia ya muda mrefu ndani ya CCM ya kutolewa kwa uamuzi mgumu katika matukio kadhaa ya kisiasa, ukiwamo ule ulioweka historia ya Aboud Jumbe kuingia akiwa Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, lakini akatoka bila cheo chochote mwaka 1984.
Pia kwenye ukumbi huo kulifanyika uamuzi wa mambo mengine makubwa, hasa nyakati za kuchuja wagombea urais au uongozi wa chama, mambo ambayo pia yanaweza kutokea katika vikao vinavyoanza leo au vya baadaye.
Alipoulizwa kuhusu kikao hicho jana, katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema Rais Kikwete ataongoza kikao cha leo kilichopangwa kuanzia saa 4:00 asubuhi na kwamba maandalizi yamekamilika, huku baadhi ya wajumbe wakiwa wameshawasili.
Alipoulizwa kuhusu nini wategemee wanachama na wananchi, Nape alijibu kwa kifupi kuwa watarajie kuwa “CCM watatoka wakiwa kitu kimoja” kuliko inavyotarajiwa na wengi.
Hata hivyo, mbali na hofu kuhusu hatua za kinidhamu kwa wajumbe walioadhibiwa kwa kuanza kampeni mapema na kukiuka maadili, taarifa nyingine kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa vikao hivyo zilidai kuwa mkutano huo utajikita zaidi kuangalia utaratibu mzima wa kuchukua fomu za wagombea wote wa urais, ubunge na udiwani.
“Vikao hivi vinaangalia utaratibu tu wa jinsi ya kuchukua fomu na wala havitagusia suala la mchujo wa wagombea urais wala ubunge,” alisema mtoa taarifa huyo.
Kamati Kuu imetanguliwa na vikao vya mfululizo vya Sekretarieti na Kamati ndogo ya Kanuni.
Kamati ya Kanuni na Maadili ilitarajiwa kukutana jana usiku au leo asubuhi kabla ya Kamati Kuu
Mtoa taarifa mwingine ambaye ni mjumbe wa NEC, alidokeza kuwa vikao hivyo havitajikita sana na uchujaji wa majina ya wagombea urais, badala yake kwa kuwa muda umekwenda, wameamua kushughulikia ratiba kwa ajili ya uchukuaji wa fomu za wagombea wa ngazi zote za uchaguzi ili nao wapate muda wa kwenda kutafuta wadhamini kabla ya mchujo.
Hata hivyo, mtoa habari mwingine kutoka ndani ya CCM, alisema licha ya kushughulikia masuala ya ratiba, kanuni na kuangalia ilani, bado suala la mchujo wa wagombea ni tata na huenda wakaangalia mgombea ambaye anaweza kukipa ushindi chama kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa huyo, hoja ya watangaza nia sita ya kukiuka kanuni za chama haitakipotezea muda, zaidi ya kuangalia nani anaweza kukipa chama ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Taarifa za ndani kutoka kwa mmoja wa wajumbe wa vikao hivyo vya juu vya CCM alidokeza kuwa kwa hali ya sasa ya kisiasa na joto linavyozidi kupanda hasa kasi ya Ukawa, CCM itafanya kama ilivyofanya kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 wakati Kamati ya Usalama na Maadili ilipokwenda Zanzibar ikiwa na faili la tuhuma za mmoja wa wagombea, lakini vikao vilijikita kwenye mgombea ambaye angekipa ushindi chama.
Kwa mujibu wa taarifa hizo mambo mengi hasa malalamiko ya ukiukwaji wa maadili wa baadhi ya viongozi ngazi za chini, yatamalizwa na Kamati Kuu na yale yatakayohitaji uamuzi wa mamlaka za uteuzi yatapelekwa Halmashauri Kuu.
Mtoa taarifa huyo alisema suala la Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Paul Makonda na makada wawili CCM, Mgana Msindai ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho mkoani Singida, na John Guninita, ambao wamefungua kesi ya madai mahakamani, linaweza kuibua mjadala.
Hivi karibuni Nape alikaririwa akisema kuwa chama hicho katika kushughulikia matatizo yote yaliyojitokeza kitatumia kanuni zake na hakuna atakayeonewa.
“Nasisitiza ni kanuni na wala si mimi, nasisitiza pia kuwa sijazuia watu kuchukua fomu bali chama kinafuata kanuni,” alisema.
Alisema kada yeyote wa CCM akiamua kufanya kampeni kabla ya muda ataadhibiwa, lakini akisubiri hana hatia kwani kinachongomba ni kanuni.
Maelezo hayo ya Nape yalikuwa yanalenga uamuzi wa Kamati Kuu ya CCM kuwafungia kwa miezi 12 vigogo wa chama hicho uliotolewa Februari mwaka jana kwa kuanza kampeni kabla ya wakati na kikiuka maadili ya chama.
Wakati huo huo, hoteli na nyumba za kulala wageni zimejaa na hiyo kufanya baadhi ya wageni wanaoingia mkoani hapa kulazimika kutafuta malazi nje ya mji.
Uchunguzi wa gazeti hili uliofanywa wa nyumba za kulala wageni katikati ya mji umebaini kuwa wageni waliojaza nyumba hizo ni wajumbe na wapambe.(Source Mwananchi)

Jumatatu, 18 Mei 2015

Mwalimu wa shule ya msingi Isagwa ajinyonga-kilolo-Iringa


 Mwalimu wa shule ya msingi Isagwa ajinyonga huko wilaya ya kilolo mkoani iringa akiwa chumbani kwake, huku akishangaza wengi siku hiyo ilikuwa ndio kikao cha mwisho cha Harusi yake, pia ameandika ujumbe unaosema nimechoka kutishiw, Mwalim huyo anayejulikana kwa jina la kisoma

Jumamosi, 16 Mei 2015

MATOKEO FORM TWO 2014 YALIYOKUWA YAMEZUIWA SABABU YA ADA YA MTIHANI


MATOKEO FTSEE 2014 YALIYOKUWA YAMEZUIWA KWA SABABU YA ADA YA MTIHANI  Bofya Hapa

SHULE ZA KIDATO CHA TANO ZIONGEZWE-RAIS

RAIS Jakaya Kikwete ameagiza Wakuu wa Mikoa na Maofisa Elimu wote nchini, kuanza ujenzi wa shule maalumu za kidato cha tano na sita kwa kila kata na wakishindwa, katika shule za sekondari za kata, wachague baadhi na kujenga madarasa ya vidato hivyo.

Alitoa agizo hilo jana katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu, yaliyoadhimishwa kitaifa katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma na kuwakumbusha kuwa kati ya wanafunzi waliofaulu kwenda kidato cha tano mwaka huu, ni asilimia 75 tu walioendelea na masomo hayo.

“Wakuu wa mikoa na maofisa elimu mliopo hapa naagiza na hili ni kwa nchi nzima, tuanze utaratibu wa kuwa na shule za kidato cha tano na sita za kata. Mnaweza kujenga shule mpya, au mchague baadhi ya sekondari za kata ziwe na kidato cha tano na sita,” alisema Rais Kikwete na kuongeza kusema si vyema kuwaacha mtaani asilimia 25 wenye sifa ya kuingia kidato cha tano.

Alisema bila kuchukua hatua hiyo, Tanzania inaweza kurudi katika hali ya elimu aliyoikuta ambapo wanafunzi wenye sifa ya kuendelea na masomo, waliachwa kutokana na ufinyu wa nafasi za kuendelea na elimu.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete, wakati alipokuwa akiingia madarakani, alikuta asilimia sita tu ya wanafunzi waliokuwa wamefanya Mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba, ndio waliokuwa wakichaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari.

“Leo kila anayefaulu darasa la saba, anakwenda sekondari… tukisema leo mwanafunzi amefeli darasa la saba amefeli kweli tofauti na zamani ambapo walikuwa wakichaguliwa,” alisema Rais Kikwete.

Tanzania ilipotoka Rais Kikwete alielezea sababu ya Serikali inayomaliza muda wake kuwekeza zaidi katika elimu, kiasi kwamba bajeti ya elimu katika Mwaka wa Fedha unaoisha kuwa kubwa kuliko ya sekta zingine, inayofikia Sh trilioni 3.4 kutoka Sh bilioni 600 iliyokuwepo mwaka 2005.

Sababu ya kwanza Rais Kikwete alisema, waliona kuwa kuwekeza katika elimu ndio kuwekeza katika taifa na Serikali isingechukua uamuzi huo, Watanzania hawataweza kutawala mazingira yao na kutumia vizuri rasilimali zao.

Pili alisema alipoingia madarakani, alikuta Tanzania yenye watu wengi zaidi katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, iko nyuma ikilinganishwa na Kenya na Uganda, kwa idadi ya wanafunzi waliokuwa wakisoma shule za sekondari na vyuo.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete, mwaka 2005 wanafunzi waliokuwa wakisoma sekondari ni zaidi ya 500,000, wakati nchini Uganda waliokuwa wakisoma sekondari walikuwa zaidi ya 700,000 na Kenya zaidi ya 900,000.

Kwa upande wa vyuo vikuu, Tanzania ilikuwa na wanafunzi 40,000 tu wakati Uganda ilikuwa na wanafunzi 124,000 na Kenya 180,000.

“Kuwa nyuma katika kutoa fursa ya elimu ikilinganishwa na wenzetu ilikuwa inaweka nchi yetu katika mazingira mabaya katika ushindani wa soko la ajira la Afrika Mashariki,” alisema Rais Kikwete.

Mbali na mazingira mabaya katika ushindani wa soko la Afrika Mashariki, Rais Kikwete alisema Watanzania nao walifikia hatua ya kuamua kupeleka watoto wao kwenda kusoma Kenya na Uganda.

Hatua zilizochukuliwa, Rais Kikwete alisema Serikali kwa kushirikiana na wananchi, waliamua kujenga shule za sekondari za kata, ambapo wananchi walihamasishwa, wakahamasika wakajenga shule mpaka Mkurugenzi mmoja wa elimu, akahofia kukosa walimu wa kupeleka katika shule hizo.

“Tulihimiza wadau wengine wajenge vyuo vya elimu ya juu na kuamua mikopo ya elimu ya juu itolewe kwa wanafunzi wa vyuo vyote,” alisema Rais Kikwete.

Alibainisha kuwa kwa sasa Tanzania ina wanafunzi 1,800,000 wanaosoma sekondari na imeshaipita Uganda yenye wanafunzi 1,700,000 wanaosoma elimu ya sekondari, lakini imezidiwa na Kenya ambayo ina wanafunzi 2,100,000.

Hata hivyo alisema ni rahisi kuipita Kenya kwa hilo pengo la wanafunzi 300,000, kwa kuwa shule za sekondari zilizopo zina nafasi ya kuongeza wanafunzi milioni mbili zaidi.


“Hapa lazima tuwafukuzie Wakenya, lazima tuwakute na kuwapita na huu ni ushindani mzuri kwa kuwa ni ushindani wa maendeleo,” alisema Rais Kikwete.

Kwa upande wa elimu ya juu, Rais Kikwete alisema vyuo vikuu vimeongezeka kutoka 26 mwaka 2005 hadi kufikia 52 na idadi ya wanafunzi walio katika vyuo vikuu ilitoka 40,719 hadi kufikia 200,956.


Chanzo:
Habari Leo

Jumatano, 13 Mei 2015

NEC sasa yaanza kugawa majimbo


TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeanza rasmi mchakato wa kugawa majimbo ya uchaguzi nchini ambapo inatarajia kuanza uchunguzi wa mipaka ya majimbo hayo hivi karibuni, ikiwa ni hatua ya maandalizi ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Aidha, tume hiyo imesisitiza kuwa uchaguzi mkuu lazima ufanyike Oktoba mwaka huu, kwa mujibu wa Katiba, na kufafanua kuwa kwa mujibu wa ratiba ya uandikishaji wapigakura kwenye daftari la wapigakura, uandikishaji huo unatarajiwa kukamilika Julai mwishoni au Agosti mwanzoni mwaka huu.
Akifungua mkutano baina ya tume hiyo na vyama vya siasa jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Damian Lubuva, alisema uchaguzi na mgawanyo huo wa majimbo unafanyika chini ya Katiba ya sasa ya mwaka 1977.
“Tume inapenda kuwahakikishia kuwa ugawaji huu wa majimbo utakamilika kwa wakati na wananchi watajulishwa ili vyama vya siasa viweze kuteua wagombea katika majimbo hayo,” alisisitiza Jaji Lubuva.
Alisema kwa sasa utaratibu wa kuandikisha wananchi kwenye daftari hilo la kudumu la wapigakura unaendelea vizuri na Serikali imeshatoa fedha zote za ununuzi wa vifaa vya kuandikishia zikiwemo BVR kits.
Alisema hadi sasa jumla ya BVR 4,800 zimeshawasili na zinaendelea kutumika katika uandikishiaji na Mei 20, mwaka huu BVR kits 1,600 zinatarajiwa kuwasili na Mei 29, mwaka huu pia BVR 1,520 zitawasili kwa ajili ya uandikishaji.
Alisema ratiba ya uandikishaji tayari imeshatoka na kwamba kwa sasa tume hiyo inaendelea kuandikisha ambapo Mei 19, mwaka huu tume hiyo itaandikisha wananchi wa mikoa ya Singida, Tabora, Igoma na Kagera na kufuatiwa na mikoa ya Shinyanga, Mwanza na Simiyu.
Aidha pia ratiba hiyo inaonesha baada ya mikoa hiyo, uandikishaji utaendelea katika mikoa ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Zanzibar na kumalizikia mkoani Dar es Salaam.
Naye Mkurugenzi wa NEC, Julius Malaba alitaja vigezo vitakavyotumika kugawa jimbo kuwa ni mgawanyo wa wastani wa idadi ya watu ambao utazingatia takwimu za idadi ya watu kutoka Ofisi ya Takwimu (NBS) na idadi ya majimbo ambayo kwa sasa ni 239.
“Kwa mujibu wa makadirio ya ofisi ya takwimu Watanzania wote Tanzania bara wamefikia milioni 47.1, kwa upande wa majimbo ya mjini yana watu takribani milioni 10 na vijijini watu milioni 37,” alisema Malaba.
Alisema kutokana na takwimu hizo, mgawanyo wa wastani wa idadi ya watu kwa majimbo ya mjini utazingatia watu 325,000 na kwa upande wa majimbo ya vijijini wastani utakuwa ni watu 250,000, hivyo majimbo yatakayogawanywa ni yale yenye idadi ya watu zaidi ya mgawanyo huo.
Alitaja vigezo kingine kuwa ni upatikanaji wa mawasiliano kama vile barabara, simu na vyombo vya habari, hali ya kijiografia kwa mfano maeneo ya mlimani, visiwani au mabondeni ni kigezo kingine cha mgawanyo wa jimbo pamoja na hali ya uchumi.
Kigezo kingine ni ukubwa wa eneo la jimbo husika, mipaka ya kiutawala, jimbo moja lisiwe ndani ya wilaya au halmashauri mbili ambapo endapo kwa sasa zipo wilaya au halmashauri zilizogawanywa, tayari zimeshatoa mgawanyo wa majimbo.
Aidha kigezo kingine ni kata moja isiwe ndani ya majimbo mawili, mpangilio wa maeneo ya makazi ya watu yaliyopo, mazingira ya muungano, uwezo wa ukumbi wa Bunge na viti maalum vya wanawake ambavyo kwa mujibu wa Katiba ya sasa ya mwaka 1977 imetenga zaidi ya asilimia 30 ya viti vya ubunge kwa ajili ya wanawake.
Alisema tume hiyo inatarajia kukutana na wadau na kujadiliana juu ya vigezo na utaratibu utakaotumika kuchunguza mipaka na kugawa majimbo, kupokea maombi na mapendekezo ya kugawa, kurekebisha mipaka au kubadili majina ya majimbo kutoka kwa wadau na kuainisha maombi hayo.
Malaba alisema tume hiyo imeweka utaratibu wa wadau kuwasilisha maombi ya kurekebisha mipaka na kugawa majimbo au kubadili majina ya majimbo ambayo yatawasilishwa kwa mkurugenzi wa halmashauri husika na kujadiliwa na vikao rasmi.
“Mkurugenzi atawasilisha maombi au mapendekezo hayo kwa Katibu Tawala wa Mkoa, ambaye atayawasilisha katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) ili kupata maoni zaidi na mwisho Katibu Tawala wa Mkoa atawasilisha maoni hayo kwa NEC,” alisisitiza.
Kwa upande wake Kamishna wa Tume, Profesa Amone Chaligha, alisema tume hiyo inatarajia kutoa ratiba kamili ya ugawaji wa majimbio hayo na matangazo yake kesho ili suala hilo, litekelezwe mapema iwezekanavyo.
Nao wawakilishi wa vyama vya siasa, akiwemo Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, na Mwenyekiti wa chama cha NLD, waliitaka tume hiyo, kuweka wazi ratiba zote zinazoendana na mchakato wa uchaguzi, ili vyama hivyo vijiandae vyema.(HABARI LEO)

welcome small city ILULA- HOME OF HOSPITALITY


Population of Ilula:

29 193 people

Latitude of Ilula:

-7,6833 (740'59.988"S)

Longitude of Ilula:

36,0333 (361'59.880"E)

Altitude of Ilula:

1 505 m

Article: Tanzania

Biggest cities: Tanzania

Photos, pictures: Tanzania

All cities: Tanzania

The biggest cities of the World

GMT time in Ilula:

+3 hours

Distance from city Ilula to 25 biggest cities of country: Tanzania

Distance (Km)
 Ilula - Dar Es Salaam  372 km
 Ilula - Unguja Ukuu  398 km
 Ilula - Mwanza  671 km
 Ilula - Zanzibar  387 km
 Ilula - Arusha  485 km
 Ilula - Mbeya  315 km
 Ilula - Morogoro  204 km
 Ilula - Tanga  447 km
 Ilula - Dodoma  170 km
 Ilula - Kigoma  774 km
 Ilula - Moshi  503 km
 Ilula - Moschi  503 km
 Ilula - Tabora  464 km
 Ilula - Songea  336 km
 Ilula - Musoma  731 km
 Ilula - Mazama  731 km
 Ilula - Iringa  38 km
 Ilula - Katumba  317 km
 Ilula - Shinyanga  531 km
 Ilula - Mtwara  539 km
 Ilula - Ushirombo  648 km
 Ilula - Kilossa  141 km
 Ilula - Sumbawanga  488 km
 Ilula - Bagamoyo  346 km
 Ilula - Bagamojo  346 km

Distance from city: Ilula to Top 10 cities of the world

Distance (Km)
 Ilula - Berlin  6 992 km
 Ilula - London  7 385 km
 Ilula - Los Angeles  16 065 km
 Ilula - Moscow  6 973 km
 Ilula - New York  12 262 km
 Ilula - Paris  7 034 km
 Ilula - Peking  9 691 km
 Ilula - Rio De Janeiro  8 565 km
 Ilula - Sydney  11 806 km
 Ilula - Tokyo  11 679 km
 Ilula - Prague  6 761 km

Jumatatu, 11 Mei 2015

Simba yaridhika Kagame na nafasi ya tatu


11 May2015
KOCHA Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic amesema anashukuru kumaliza ligi katika nafasi ya tatu na sasa anasubiri hatima yake.
Simba ilimaliza ligi juzi kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya JKT Ruvu na kumaliza ya tatu ikiwa na pointi 47.
Kopunovic alianza kuiongoza Simba mwishoni mwa raundi ya kwanza akichukua mikoba ya Patrick Phiri aliyetupiwa virago baada ya timu kutopata matokeo mazuri.
Akizungumza na gazeti hili jana, Kopunovic alisema ligi ilikuwa na changamoto nyingi na kumaliza nafasi ya tatu ni jambo la kushukuru.
“Halikuwa lengo letu, wote tulitaka kutwaa nafasi kubwa zaidi, lakini ligi ilikuwa na changamoto nyingi, nitakabidhi ripoti yangu kwa uongozi, hapo ndipo utajua hatima yangu,” alisema kocha huyo aliyesaini mkataba wa mwaka mmoja na Simba.
Akilizungumzia hilo, msemaji wa Simba Haji Manara alisema wanachokisubiri ni kuona ripoti ya kocha huyo kabla ya kufanya uamuzi mwingine.
“Watu wana papara ya kutaka kujua nini kitafuata, tumeshiriki ligi kama timu nyingine na yaliyotokea yametokea, kiutaratibu tunasubiri ripoti ya kocha ndipo mambo mengine yafuate kama kusajili ama la,” alisema.
“Tunataka tuwe na uhakika wa nini tunataka kufanya, kama mabadiliko ni yapi, yote hayo tunayafanya kwa muongozo wa ripoti ya kocha,” alisema Manara.
Hata hivyo, taarifa za ndani ya klabu hiyo zinasema, Simba imepania kufanya mabadiliko katika kikosi chake ili kumaliza kwenye nafasi zitakazowawezesha kushiriki michuano ya kimataifa baada ya kuikosa kwa mwaka wa nne sasa.

USAJILI: Simon Msuva aiangukia Yanga

Msuva 
Na Khatimu Naheka na Iman Makongoro, 
Kwa ufupi
  • Ukiacha Nonda Shaaban ‘Papii’, hakuna mchezaji mwingine aliyefanikiwa kung’ara au kuuzwa nje ya nchi akitokea Yanga.

Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva amereja nchini akitokea Afrika Kusini kufanya majaribio ya soka la kulipwa na amewaangukia viongozi wake kutofanya makosa ya kuzuia uhamisho wake.
Msuva mfungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara, katikati ya wiki iliyopita alitoroka na kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio katika klabu ya Bidvetes Wits inayoshika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu nchini humo ikiwa na pointi 52 juu ya Mamelodi Sundowns 57 na vinara Kaizer Chiefs wenye pointi 69.
Akizungumza na gazeti hili mara baada ya kuwasili juzi, Msuva alisema amefanikiwa kuandika historia katika maisha yake ya soka kwa kufanya majaribio katika klabu ya Wits na sasa anasubiri majibu ya majaribio hayo kabla ya kuanza mchakato wa uhamisho.
Msuva ambaye amefunga mabao 17 katika Ligi Kuu msimu huu alisema anauomba uongozi wa klabu yake chini ya mwenyekiti Yusuf Manji kutoweka ugumu katika uhamisho huo badala yake wafanye taratibu nyepesi ili aweze kucheza soka nje ya Tanzania.
“Unajua haya ni maisha na hii ni nafasi yangu ya pekee niliyopata, nashukuru kila kitu kilienda sawa, ombi langu kwa uongozi ni kunisaidia nikamilishe ndoto yangu,”alisema Msuva.
“Uongozi ningeuomba endapo hawa jamaa (Wits) watakuja kuanza mchakato wa usajili wasiwe na tamaa ya fedha kwa kutaja kiasi kikubwa ambacho kitakwamisha uhamisho wangu.”
Katibu Mkuu wa Yanga, Jonas Tiboroha alilithibitishia gazeti hili jana kuwa  hawana mpango wa kumuwekea vikwazo Msuva huku akibainisha kuwa wanachohitaji ni taratibu zifuatwe ingawa hadi jana mchana hakuna kiongozi wala wakala wa klabu ya Bidvest aliyewafuata.
“Kama kweli wana nia na Msuva, tuko tayari kumwachia akatafute maisha mengine ya soka nje ya nchi, madai kuwa tuna mpango wa kuweka dau kubwa ili kumkomoa si kweli, tutaweka dau ambalo kwetu tunaona ndilo linafaa kumuuza Msuva,” alisema katibu huyo.
“Kama timu inayomtaka itashindwa dau letu basi haimuhitaji, mbona kuna wachezaji wanauzwa hadi dola milioni moja, dola laki saba na kuendelea? Hivyo Msuva ‘akithitibisha’ anaweza, fedha tunayoitaka haitakuwa ya kushtua,” alisema Tiboroha bila kubainisha ni kiasi gani.
Tiboroha alisema walitarajia kukutana na Msuva jana jioni ili kujua hatma yake endapo anaondoka Yanga au la.
Yanga imekuwa na tabia ya kuwazuia wachezaji wake wanapotakiwa na klabu mbalimbali nje ya nchi, ilishafanya hivyo kwa Jerryson Tegete na Mrisho Ngassa na Haruna Niyonzima.
Mwaka 2009, Ngassa alitakiwa bila ya kufanya majaribio katika  klabu ya Lov-Ham ya Norway kwa gharama ya Dola za Marekani 50,000, lakini Yanga walisema klabu yao ni kubwa ambayo haina shida na ina uwezo wa kuwalea wachezaji wake na ndiyo maana haipo tayari kuwauza nyota wake kwa bei rahisi na pengine wangelipwa zaidi ya Dola za Marekani 100,000 wangeweza kumwachia.(Mwananchi)

New S. African Democratic Alliance Leader Rejects ‘Token Black' Label

Newly-elected Democratic Alliance (DA) party leader Mmusi Maimane, delivers his victory speech May 10, 2015, in Port Elizabeth, South Africa.
Newly-elected Democratic Alliance (DA) party leader Mmusi Maimane, delivers his victory speech May 10, 2015, in Port Elizabeth, South Africa.
South Africa's main opposition party, the Democratic Alliance (DA), has elected its first black leader.  Mmusi Maimane takes over from Helen Zille, who has been at the helm of the party for eight years.
At 34 years of age, the charismatic politician known for his sharp oratory skills and slick campaigns is often dubbed the “Obama of Soweto."
Mmusi Maimane pushes away such comparisons, but observers say his appointment as the new leader DA party could help shift a political landscape that currently tilts heavily in favor of the ruling African National Congress (ANC) party.
The eldest of four siblings, Maimane was born in Krugersdorp and brought up in Soweto - a township on the edges of Johannesburg that became the political epicenter of the anti-apartheid struggle.
Maimane joined the DA in 2010. He quickly rose through the ranks to become the party’s national spokesman in 2011.  Last year, he lost his bid to lead the provincial government of South Africa's wealthiest province, Gauteng.
As the party's parliamentary leader, he accused President Jacob Zuma of being a “thief” during a heated parliamentary debate in March.  His colleagues say he has a good sense of humor but is an “absolute perfectionist."
On May 10, Maimane became the DA’s first black party leader during a party conference with 88.9 percent of the vote.
Despite the DA’s growth in the last few elections – 12.4 percent of the vote in 2004, 16.7 percent in 2009 and 22.2 percent in 2014 – the party is still considered “too white” to threaten the supremacy of the ruling ANC, says political analyst Nic Borain.
Electing Maimane as party leader is one of several steps the DA is taking to enable it to dig into the ANC’s core constituency, Borain says.
“Mmusi is very specifically tailored.  He was chosen and his rise was so quick because he fits exactly the profile the DA wants.  His appointment is a necessary but not sufficient condition for the DA to break out of its racial confines.  Mmusi is the transitional object,” says Borain.
Maimane has a bachelor's degree in psychology from the University of South Africa and a master’s degree in theology from Bangor University in the United Kingdom.
Before getting into politics, the gangly, eloquent leader - included in GQ magazine's 2014 list of best-dressed men - lectured at a business school in Johannesburg.  A devout Christian, he is a preacher at the charismatic Discovery Church in Randburg.
Borain says it’s Maimane’s “popular appeal” the DA is hoping to capitalize on.
“Electing a leader who is a preacher in charismatic churches is a particular kind of appeal which the DA historically shied away from – a popular appeal.  I think it is part of the compromises the DA is prepared to make with its principled ideology historically to reach new voters, new young black voters,” says Borain.
The ANC has said that he is too young and that his rapid elevation is a symptom of racial tokenism – a label flatly rejected by Maimane’s colleague and shadow minister for public enterprises, Natasha Michaels.
“Calling Mmusi a token black is an absolute insult.  I think the fact that he received the overwhelming landslide victory that he did proves that black, white, colored, Indian, Asian – we all agreed that he was the man for the job and he was the man to take us forward,” said Michaels. “The energy of his age is going to be a huge advantage. He brings a certain dynamic to parliament that is desperately needed because we are a very young country," added Michaels.(source VOICE OF AMERICA)

Ijumaa, 8 Mei 2015

SHERIA YA MAKOSA YA MITANDAO TAYARI IMESAINIWA NA RAIS

Rais Jakaya Kikwete tayari ameshasaini sheria yenye utata ya makosa ya mtandao na muda wowote kuanzia sasa itaanza kutumika rasmi
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, amesema hayo leo wakati akizungumzia masuala mbali mbali yanayohusu sheria hiyo ambayo kupitishwa kwake kumesababisha malalamiko mengi kutoka kwa wadau kuwa itaminya uhuru wa habari, kuingilia faragha pamoja na uhuru wa watu kuwasiliana.
Huu ni uchambuzi kidogo kuhusu baadhi ya vipengele vilivyozua utata katika muswada uliokuwa umetolewa
1. Kifungu 7 (2b): Mpokeaji wa ujumbe (receiver) anaweza kushtakiwa kwa kosa la kupokea ujumbe ambao sheria imeufanya kuwa wa jinai. (Mfano: Mtu akikuforwadia ujumbe, ukiupokea na wewe umefanya kosa la jinai).
2. Kifungu 8: Itakuwa ni kosa la jinai kama mtu ataweka wazi nyaraka za siri za serikali hata kama ni nyaraka ya kusaidia nchi kwa ujumla (Mfano: Matumizi mabaya ya mali ya umma).
3. Kifungu 14: Picha yoyote yenye mwelekeo unaoweza kuonekana kama ‘mchafu kingono’ inaweza kupelekea mtu kufungwa hadi miaka 10 au kulipa milioni 30; (Mfano: mtu kaposti picha yake ambayo sio ya ponografia lakini ‘ikatafsiriwa’ hivyo. Sheria haijatafsiri ponografia!)
4. Kifungu 23: Je, ulijua kuwa ‘kusababisha maudhi ya hisia’ kwa mtu mwingine ni unyanyasaji na unaweza kufungwa kifungo kisichopungua mwaka mmoja?
5 Kifungu 22: Ukiweka ujumbe katika mtandao na ukaufuta au kuuboresha, kama ukishtakiwa kwa kuweka ujumbe huo unaweza kuhukumiwa pia kwa adhabu ya kuuboresha au kuufuta. (Mfano: unapofuta ‘status’ zako za WhatsApp, unaweza shitakiwa kwa kuchelewesha ushahidi kisa tu ulifuta na hamna mtu anayeweza kujua ulifuta kwa kusudi au la.)
6. Mkuu wa kituo cha Polisi chochote kile nchini anaweza kuagiza wewe umpatie simu/laptop yako au taarifa zako zote (kwenye email, chats) au hata vifaa vyako au ofisi yako kwa ajili ya upelelezi bila oda ya Mahakama.
7. Serikali kupitia waziri husika ndio ina mamlaka ya kusema jambo lililowekwa kwenye mtandao ni la kweli, uongo au la kupotosha(SOURCE:East Africa Television (EATV)

Alhamisi, 7 Mei 2015

huyo ndo rais mpya aliyechaguliwa DARUSO-MUCE

SHAMRA SHAMRA ZA USHINDI 
 Baada ya kampeni zilizo dumu kwa wiki moja, wanafunzi wa chuo kikuu Dar es salaam kitivo cha uwalimu Iringa (MUCE) wamefanya uchaguzi leo, Kwa hali ya amani na utulivu wa hali ya juu na hatimaye kuwapata viongozi wa serikali yao, Uchaguzi huo uliokuwa unawagombea zaidi wawili  katika kila nafasi ulilazimu kuwachukuwa siku nzima kufanyika na hatimaye Bw. BAKARI, IBRAHIMU ameibuka mshindi katika nafasi ya urais, Kwa matokeo mengine ungana nasi kesho

 

Mrema avuliwa uanachama TLP

Mrema avuliwa uanachama TLP

mrema
NA SHABANI MATUTU, DAR ES SALAAM
KAMATI ya Ukweli na Maridhiano ya Chama cha Tanzania Labour (TLP), imetangaza kumvua uanachama Mwenyekiti wa chama hicho, Agustino Mrema.
Akizungumza jana, jijini Dar es Salaam na MTANZANIA Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Joram Kinanda alisema kuwa kamati hiyo imefikia uamuzi huo baada ya kupitia kwa kina malalamiko yaliyokuwa yakimuhusu Mrema, ambaye pia ni Mbunge wa Vunjo.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa mbali na Mrema wengine waliovuliwa uanachama ni Hamisi Mkadamu, Antoni Mapunda, Nancy Mrikaria, Dominata Rwechungura, Maxmilian Lymo, Richad Lyimo, Hamisi Mkumba na Stanley Temba.
Kinanda alisema kuwa wanachama hao wamevuliwa uanachama kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, toleo la 2005 Ibara ya 9.9 (c) na 2009 ibara 9.5(c).
Kinanda alisema kuwa maazimio hayo yamepelekwa katika ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kwa taratibu za kisheria pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Kwa upande wake Msajili Msaidizi wa Vyama Vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza, alipotafutwa ili kupata ufafanuzi wa suala hilo, alisema kamati hiyo haitambuliki kisheria.
“Kamati hiyo haitambuliki kisheria, na hata Mrema mwenyewe amekuwa akipinga TLP kuwa na kamati ya aina hiyo na hata viongozi wake hawatambuliki, ” alisema(Chanzo Mtanzania)


Jumanne, 5 Mei 2015

Madereva wasitisha mgomo, mabasi ya mikoani yaanza kazi


Mbowe akizungumza na madereva mara baada ya kuwasili katika kituo cha mabasi cha Ubongo leo jijini Dar es Salaam.  
Na Online Team, Mwananchi

Posted  Jumanne,Mei5  2015  saa 8:24 AM
Kwa ufupi
Mgomo huo ulioanza jana umesababisha usumbufu mkubwa kwa raia sehemu nyingi nchini Tanzania ambao walikuwa wamejiandaa kusafiri kuelekea katika mikoa mingine jana na leo kwa ajili ya shughuli zao mbalimbali zikiwemo za kibiashara na kijamii.
Hatimaye madereva wa mabasi na malori wameamua kusitisha mgomo leo baada ya Serikali kuwahakikishia kuwa inaandaa utaratibu mzuri wa kujibu na kushughulikia matatizo yao.
Mgomo huo ulioanza jana umesababisha usumbufu mkubwa kwa raia sehemu nyingi nchini Tanzania ambao walikuwa wamejiandaa kusafiri kuelekea katika mikoa mingine jana na leo kwa ajili ya shughuli zao mbalimbali zikiwemo za kibiashara na kijamii.
Taarifa zilizotufikia ni kwamba Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akiwa na viongozi wengine wa Serikali walifika katika kituo cha mabasi yaendao mikoani cha ubungo na kuzungumza na madereva hao wakiwataka wasitishe mgomo wao na kuanza kazi kwani mambo yao Serikali inayafanyia kazi na hivi karibuni watajibiwa.
Kufuatia hali hiyo maderva hao walikubaliana na ombi hilo la Serikali baada ya kutokea kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe ambaye naye aliwasihi waache mgomo huo kwani Serikali itafanyia kazi maombi yao.
Nchi yasimama: Madereva mabasi, malori wagoma sehemu kubwa ya Tanzania
Dar/mikoani. Nchi imesimama. Hii ndiyo sentensi inayofaa kuelezea tukio la jana la mgomo wa madereva nchini kote ambao kwa mara ya kwanza ulisababisha mabasi yote kutoka Dar es Salaam kwenda mikoani na nchi jirani kushindwa kuondoka.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT), kushindwa kutoa huduma kwa sababu yoyote ile.
Tangu asubuhi hadi jioni, hakuna basi hata moja lililotoka wala kuingia katika kituo hicho hadi abiria walipoanza kukata tamaa na baadhi yao kuondoka na wengine kuanza kushinikiza kurejeshewa nauli.
Mgomo huo ambao ni mwendelezo wa ule uliofanyika Aprili 9, mwaka huu ulipewa uzito na madereva hao baada ya ahadi walizopewa na Serikali kutofanyiwa kazi kama ilivyoahidiwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka.

Hata hivyo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameunda kamati ya iliyotangazwa na Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta ya kusimamia usafiri barabarani itakayowakutanisha wadau wote ili kutatua matatizo katika sekta hiyo kila yanapotokea.
Polisi wachemsha Dar
Tangu saa 2.30 asubuhi, polisi walijaribu kuyasindikiza mabasi waliyodhani madereva wake wako tayari kuondoka Ubungo lakini walishindwa baada ya kutoungwa mkono.
Mkuu wa Trafiki Ubungo, Inspekta Yussuf Kamotta akiwa na Inspekta Solomon Nkindwa ambaye pia ni mkaguzi wa magari, waliingia katika basi la Kampuni ya Master City na kuliondoa kituoni hapo wakiwa na mmiliki wa kampuni hiyo, Abdallah Mohammed huku wakimtafuta dereva bila mafanikio na kulazimika kulitafutia sehemu salama ya kuliegesha baada ya madereva kulizingira.
Kitendo cha askari hao kilisababisha kuzomewa kwa Inspekta Nkindwa wakisema mkaguzi huyo arudi shule akasome... “Solomoooon… rudi shuuuule… gia nane… zimekushinda,” walisikika madereva hao wakiimba huku wakikimbia mchakamchaka kurudi zilipo ofisi zao.
Kutokana na vurugu zilizotokea nje ya kituo hicho, polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya watu waliokuwa katika makundi.
Nje ya UBT, magari sita ya polisi yaliegeshwa katika makutano ya barabara za Sam Nujoma, Nelson Mandela na Morogoro wakati mengine yakielekea Mwenge na Buguruni kwenda kukabiliana na tishio lolote ambalo lingeweza kutokea.
Saa 5.30 askari wa Kikosi cha Mbwa waliwasili kuongeza nguvu na kuvutia macho ya wengi kutokana na jinsi walivyokuwa na pilikapilika bila ya kuwapo kwa mhalifu yeyote anayetafutwa.
Sikukuu ya madereva
Tofauti na migomo mingine, huu haukuwa na vurugu zozote wala sintofahamu kwani kila mtu aliyekuwa UBT alionekana akiwa katika sehemu yake akiendelea na hamsini zake. Abiria walikuwa katika mabasi husika huku mawakala na makarani wakiendelea kukatisha tiketi za safari na kupanga mizigo ya abiria.
Huku wakiendelea na mazungumzo yao katika vikundi katika kituo hicho, madereva hao walisikia wakisema hapakuwa na mgomo, bali sikukuu yao.(CHANZO MWANANCHI)

ANGALIZO ..............

Ndugu watazamaji wa blog hii, blog hii imeanzishwa kwa lengo la kufikisha ujumbe kwa jamii,kutoa taarifa na kuonya,  kutoa maoni na kama unatangazo lolote huna budi kuwasiliana nasi 

lakini sio kutaka kile wanachokitaka watu wachache kwa hiyo kama kuna tatizo wasiliana nasi na si kulaumu na kuchafua chombo husika, .

TANGAZA BIASHARA, TAARIFA NA MAELEZO WASILIANA NASI.

Jumamosi, 2 Mei 2015

KAMPENI ZA UCHAGUZI KUTOKA CHUO KIKUU KISHIRIKI MKWAWA 2015

KAMPENI ZA UCHAGUZI KUWANIA UONGOZI KATIKA SERIKALI YA WANAFUNZI ZAENDELEA KWA MBWEMBWE

 

Serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Mkwawa (DARUSO-MUCE) imemaliza muda wake na hivyo iko katika mchakato wa kutafuta Rais mpya wa serikali hiyo pamoja na wabunge watakaongoza serikali hiyo kwa kipindi cha 2015/16 Chuoni hapo.
Aidha kampeni za mgombea Urais ndugu BAKARI, IBRAHIMU zimeonekana  kuwawavutia wanafunzi wengi kwani amekuwa akitembelea wapiga kura wake huku akiwa ameandamana na wafuasi  wake ambao wamekuwa wakimlinda kila anapokwenda. Aidha mgombea huyo Bw. BAKARI, IBRAHIMU ndie ambae anaonekana ni mwenye asilimia kubwa ya kuweza kushinda katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika wiki lijalo chuoni hapo. Wagembea wengine ni; MSUYA, FAROUK na Bw MABULA

WAGOMBEA URAIS DARUSO MUCE 2015/2016.....................

Na kwa upande wa makamu wa rais wagombea wawili wamejitokeza  akiwamo dada ISSASSI SUZANI na KIBONA FAUSTA katika nafasi hii ushindani unaonekana kuwa ni mkubwa sana kwani wote wana watu weng wanaowapigania ili kupata nafasi hiyo




WAGOMBEA WA NAFASI YA MAKAMU WA RAIS DARUSO-MUCE 2015/2016

Mgombea wa nafasi ya Rais Bwana BAKARI, IBRAHIMU  sera zake kwa wapiga kura (hawapo pichani) ambapo alisema katika uongozi wake ataanza kushughulikia mikopo kwa wanafunzi wa MUCE.
Pia amesema kama atapewa nafasi hiyo atakuwa na utaratibu wa kuwakutanisha wanafunzi wa MUCE kuanzia mwaka wa kwanza mpaka wa tatu na wataalumu waliopo katika fani zao, lengo likiwa ni kuwaongezea uzoefu zaidi na kujua changamoto ya kazi za kitaaluma chuoni hapo.
Aidha aliongeza kuwa atahakikisha usiri wa matokeo utaboreshwa chuoni hapo, huku akimwaga ahadi ya hakuna tatizo ambalo hawezi kulishughurikia akiwa rais na hii ilikuja baada ya mheshimiwa kitako kumuuliza mgombea matatizo gani manne(4)  hawezi kuwasaidia wanachuo akiwa madarakani.

Wanafunzi hao wameonekana wana ukomavu mkubwa wa kisiasa kwani wanasikiliza kwa makini sera za wagombea na kuuliza  maswali mazuri.
Cha kufurahisha ni kelele za filimbi na mayowe ambayo yametwala kila kona huku wagombea wakishangiliwa na mashabiki wao.

Nafasi zinazowaniwa katika Uchaguzi huo ni pamoja na nafasi ya Rais, Makamu wa Rais, pamoja na wawakilishi wa Vitivo (wabunge) na wawakilishi wa Maeneo (wabunge wa makazi) ambao wote watapigiwa kura.
Wagombea mbalimbali wamekuwa wakipita hapa na pale ikiwa ni pamoja na kubandika picha zao katika kuta ikiwa ni sehemu ya kutafuta kura.
Kwa upande wa MSUYA  naye amenadi sera sake moja ya mipango yake ni kushughulikia matatizo mbalimbali ya wanafunzi likiwemo tatizo la maji na tatizo la umeme kukatika mara kwa mara, huku akiwasii wanafunzi kuangalia hali ya chou sasa kwamba kinahitaji mtu makini anayejua matatizo ya wanachuo wote na kuwatumikia.
KWA UPANDE WA MAKAMU WA RAIS SERA ZAO IMEONEKANA KWENDA SAMBAMBA NA MARAIS lengo kubwa ni kuboresha taaluma na mazingira y chuoni hapo.

Kwa upande wake Rais anayemaliza muda wake Bwana AGUSTINO ALFA ameishukuru tume ya uchaguzi kwa mchakato mzima na anafurahi kumaliza muda wake na kuwataka watakaopata nafasi za kuongoza wazingatie sheria, demokrasia na upendo ili kuleta mshikamano katika chuo, ili wanaoongozwa wajisikie kuwa na amani kuwepo chuoni hapo badala ya kutatua migogoro isiyokuwa na maana. Pia ameshauri wanachuo kusikiliza sera za wagombea kwa umakini mkubwa ili kuepuka KUUZIWA MBUZI KWENYE GUNIA.
 
 MSHAURI WA WANAFUNZI ALITUMIA FURSA HIYO KUWAASA WAGOMBEA KUTUNZA MAZINGIRA HASA KUTOBANDIKA MABANGO SEHEMU ZISIZO RASMI
                                         NAYE MAKAMU WA CHUO AKASEMA;
Makamu mkuu wa chuo amewatakia wanafunzi kampeni njema zenye baraka na fanaka na zinazozingatia sheria na taratibu za chuo.