ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatano, 6 Aprili 2016

UPINZANI WAPEWA NAFASI ZANZIBAR


RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ameteua wanasiasa saba kuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakiwamo watatu waliowania Urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa marudio wa Machi 20, mwaka huu.
Hao ni aliyekuwa mgombea wa nafasi ya urais wa chama cha ADC, Hamad Rashid Mohammed, Said Soud Said aliyewania nafasi ya urais kupitia AFP Wakulima na Juma Ali Khatib wa ADA-TADEA.
Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari, wengine walioteuliwa ni Balozi Ali Karume, Waziri wa zamani wa Fedha na Uchumi katika Serikali ya Rais mstaafu Dk Salmin Amour, Balozi Amina Salum Ali pamoja na Mohamed Aboud Mohamed aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
Pia yumo Mouldine Castico ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katika hotuba yake ya uzinduzi wa Baraza la Wawakilishi, Rais Shein aliahidi kuunda serikali itakayovishirikisha vyama vya siasa kwa ajili ya kuleta maendeleo ya wananchi wote bila ya kujali itikadi za kisiasa.

Hakuna maoni: