ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 29 Aprili 2016

Spika apangua tena Kamati za Bunge


SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amepangua tena Kamati za Kudumu za Bunge huku akiagiza Ofisi ya Katibu wa Bunge kuratibu uchaguzi wa kamati sita. Kwa mujibu wa Waraka Na 04/2016 wa Mabadiliko ya wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge uliotolewa jana hapa, Spika pia amefanya mabadiliko ya wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge.
Spika Ndugai alisema Ibara ya 96 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imelipa uhalali Bunge kuunda Kamati za Bunge za namna mbalimbali kadri itakavyoona inafaa kwa ajili ya utekelezaji bora wa madaraka yake.
Alisema pia kwa mamlaka aliyopewa chini ya Kanuni ya 116 (3) na (5) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Aprili 2016, amelazimika kufanya mabadiliko ya wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge.
Spika alisema sababu kubwa iliyomfanya kufanya mabadiliko hayo ni kuhakikisha kuwa kila mbunge ikiwa ni pamoja na wabunge wanne wapya walioapishwa Aprili 19, anakuwa mjumbe kwenye kamati mojawapo ya Bunge.


Alisema aidha mabadiliko hayo ni kwa ajili ya kuhakikisha pia kuwa kwa kadri inavyowezekana, muundo wa Kamati za Kuduma za Bunge unazingatia aina za wabunge (jinsia, pande za Muungano na vyama vya siasa vyenye uwakilishi bungeni), ujuzi maalumu, idadi ya wajumbe kwa kila kamati na matakwa ya wabunge wenyewe.
Aliwataja wabunge walioapishwa kuwa ni Shamsi Vuai Nahodha na wabunge wa Viti Maalumu, Ritha Kabati (CCM), Oliver Semuguruka (CCM) na Lucy Owenya (Chadema). Wabunge waliobadilishwa ni Neema Mgaya kutoka Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwenda Huduma na Maendeleo ya Jamii, Bernadeta Mushashu kutoka Ardhi, Maliasili na Utalii kwenda Huduma na Maendeleo ya Jamii na Kunti Majala kutoka Ardhi, Maliasili na Utalii kwenda Kilimo, Mifugo na Maji.
Wengine ni Ussi Salum Pondeza kutoka Nishati na Madini kwenda Katiba na Sheria, Richard Ndassa kutoka Katiba na Sheria kwenda Ardhi, Maliasili na Mazingira, Sebastian Kapufi kutoka Utawala na Serikali za Mitaa kwenda Ardhi, Maliasili na Utalii.
Mabadiliko hayo pia yanawahusu Atupele Mwakibete kutoka Sheria Ndogo kwenda Ardhi, Maliasili na Utalii, Omar Kigoda kutoka Miundombinu kwenda Ardhi, Maliasili na Utalii, Dk Godwin Mollel kutoka Katiba na Sheria kwenda Ardhi, Maliasili na Utalii, Dk Raphael Chegeni kutoka Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwenda Viwanda, Biashara na Mazingira, Ibrahim Hassanali Raza kutoka Utawala na Serikali za Mitaa kwenda Viwanda, Biashara na Mazingira na Abdulaziz Abood kutoka Hesabu za Serikali za Mitaa kwenda Viwanda, Biashara na Mazingira.
Wengine ni Emmanuel John kutoka Utawala na Serikali za Mitaa kwenda Kilimo, Mifugo na Maji, Jacqueline Msongozi kutoka Huduma na Maendeleo ya Jamii kwenda Hesabu za Serikali za Mitaa, Josephine Genzabuke aliyetoka Huduma na Maendeleo ya Jamii kwenda Hesabu za Serikali na Suleiman Sadick kutoka Huduma za Maendeleo ya Jamii kwenda Viwanda, Biashara na Mazingira.
Kwa upande wa wabunge walioapishwa na kupangiwa kamati ni Nahodha aliyepangiwa Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Owenya Ardhi, Maliasili na Utalii, Kabati Miundombinu na Semuguruka Kilimo, Mifugo na Maji.

Hakuna maoni: